Elections 2015 Yaliyojiri katika vikao vya CCM Dodoma - Julai 10-12, 2015. Magufuli achaguliwa kuwa mgombea Urais

siamini , ngoja nisubiri taarifa rasimi ta kutoka kwa ndugu Nape Nnauye
 

sasa hizi kelele zote ulizoandika hapa siungeweka tu hiyo habari yako?
 

km ulikuwa ushazaliwa mwaka 1995 wakati mkapa ni mgombea wa ccm,upande wa pili alikuwa mrema,hayo unayosema nayo yalisemwa......ila nadhani ushasoma historia umeelewa nn kiltokea.
 
makufuli ana advantage sana

Ni kweli, kwa mtizamo wa kutuliza kichwa CCM watakuwa wamefikiria mambo mengi, hasa kujaribu kupunguza nguvu ya CDM kanda ya ziwa na pia kutokuwa na makundi kutamsaidia pengine kupata support hata kwa waliokatwa wenye makundi.
 
Membe mfumo umemwandaa kwahiyo hana mpinzani kama unabisha kula jiwe uone.
 
Ccm hakuna rais hapo tutawachakaza kwa kutumia dume ukawa lazma wapelee
 
Wewe mburulaa kweli! Hapo watakao enguliwa ni Membe na Asha huku amina akiwa Makamu. Huyo Dogo January atalamba pengine uPM

mkuu unaweza kwenda mbali zaid utwambie hawa wataenguliwa kwa kura ngapi na hawa washindi watashinda kwa kura ngapi ili nisihangaike ata kupiga kura??
 
2015 ilipaswa iwe zamu ya Zanzibar!, Jee kwa majina haya, jee bado kuna uwezekano wa Zanzibar kupatiwa haki yake?!.

Pasco

Mkuu Pasco habari ya Asubuhi,

Wewe ni mtu wa karibu na Lowassa au kambi ya Lowassa, hebu nijuze mkuu, Lowassa na Timu yake wako ktk hali gani kipindi hiki? Wameyapokeaje matokeo haya? Au ile kamati ya Maridhiano omefanya kazi yake na hivyo tuterajie mzee akipewa sehemu ya kurudisha gharama alizotumia kwenye maandalizi ya uchaguzi huu? Kwamba tujiandae kwa Ka-Escrow, Richmond kengine?

Mkuu ninaamini lazima utakuwa na taarifa moja au zaidi kuhusiana na hili.!!

BACK TANGANYIKA
 
Magufuli ni Mikoba ya JK Hawezi Kumpitisha Sababu Tayari ni Mtumwa wa JK, Atakepitishwa ni Membe. Magufuli ni PM, Kama CCM Ikishinda hiyo Octoba.
 
Cc Pasco karibu Ukawa tusake mabadiliko mmeyakosa ccm .Mzee AMESHAKATWA
 
Last edited by a moderator:
Kutoka Safari ya matumaini hadi Safari ya Majonzi..

Pamoja na wadhamini Laki 8 lkn bado umekatwa.. Pole sana brother nenda Monduli ukacheze na wajukuu zako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…