Yaliyojiri Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, kesi ya Mbowe na wenzake 3 - Kesi imeahirishwa hadi Nov. 29 2021

Wazazi wako wamepata faida kubwa mno kuwa na mtoto kama wewe.
Umeandika na kuchambua kwa haki na ukweli kabisa,kwa weledi na ufasaha mkubwa mno.
Ukweli hua haufichiki.
Nawapongeza wazazi wako kwanza na sasa nakupongeza wewe pia.
 
Naona mtanange umenoga sana. Palipofika ni patamu na patampa taabu sana jaji

Jinsi nilivyousoma huu mchezo, ni kwamba barua au document mawakili wa utetezi wanayotaka mahakama ihipokee haina tatizo hata kidogo. Mawakili wa jamuhuri wanaona kwamba ikipokelewa inaweza ikawa ndio mwisho wa kesi kwani mambo aliyoomba Lingwenya athibitishiwe kama Kweli alipelekwa central polisi na si Tazara litawaletea shida na itajulikana kuwa hii kesi ni ya kubumba

Nampa salute aliye format hiyo barua.
 
Halafu Jaji kwanini kila Hoja lazima Ahirishe Mahakama? Anatumia huu muda kwenda kupata Maagizo toka kwa Wakubwa wake? Hizi mbona alisha zitolea maamuzi kama Mara 2/3 wakati Akina Kibatala na wenzie wanapinga Baadhi ya Vielelezo visipokelewe. Sasa the Same Scenario anaahirisha Kesi? Mmmmmmh Huyu Jaji.

Sijui Ngoja Tuone
 
Da! Huku kuandika bila kusoma kwanza comments si kitu kizuri. Ingawa tulikuwa na mawazo sawa ila wewe jamaa nakupa saluti. Umeelezea vizuri mnoooo
 
Lisu yuko nao,Wanawasiliana.Hii kesi upande wa utetezi wamejipanga Sana.Fikiria jinsi walivyoshitukizwa Jana na bado wakaunganisha utetezi ulioleta kizazaa mahakamani.
Imepelekea watu wamepanic huko hadi wanaongea maneno bila utaratibu.Tunaomba haki itendeke na ionekane ikitendeka kwa ajili ya maslahi mapana ya Taifa letu.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Mimi nahisi mojawapo ya haya linaweza kutokea j3 ijayo:
[emoji106]Mwamuzi anaweza akapata dharula itakayomfanya ashindwe kuja mahakamani j3
[emoji106]Mwamuzi anaweza akaamua kujitoa weekend hii na j3 akaenda kutangaza uamzi wake
[emoji106]Dipipiii anaweza akatangaza kutokuwa na nia ya kuendelea na hii kesi
[emoji106]Mwamuzi anaweza kuamua barua ipokelewe na koti japo ni rahisi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko hicho kijikaratasi kupokelewa na koti; na
[emoji106]Mwamuzi anaweza akaamua kwa kutumia kigezo almaarufu cha "kwa maoni yangu" kuipa ushindi sirikali (na hili ndilo linalodhaniwa kwamba ndilo litakalotokea).

Yamkini naweza nisiwe sahihi sana lakini hayo ndiyo maoni yangu.
 
Imagine hawapata muda wa kupewa taarifa kwamba kesho utetezi mnaanza, ila ushahidi wa ling'wenya tu jaji anakurupuka eti shahidi anapewa majibu!
 
Mawakili wa Serikali kwa nini wanaogopa barua hii isipokelewe?
Akili kichwani mwako, tukutane Monday!!
Wamepanic wanaogopa maana wanajua vyote ni vya kifundishwa hakuna kesi ya kueleweka apo na ndo maana juzi hawakusema wamemaliza ushahidi ili tu wasiwape muda mawakili wa utetezi kujiandaa lakini bado utetezi walikuwa tayari kwa lolote adi jaji anakurupuka eti shahidi anapewa majibu!
 
Hakuna kesi apo ni dhuluma tu wameamua kufanya wanajisahau wanajiona miungu watu! Toka kesi imeanza ushahidi ni kukamata tuu kukamata, tukawapeleka wapi sjui, ila vitendo vya ugaidi vyenyewe havimo sa sjui watakuja kuvieleza kwamba wamefanya wakiwa magereza??
 
Picha inayojitengeneza iko hivi:

Makomandoo, warriors, Adamoo, Lijenje, Lingwenya na wengine, walifundishwa na Luteni Denis Urio medani za kivita na za kikomandoo na wakaiva vizuri. Ujue kuna bonding inatokea wakati vijana kakamavu wanapofanya mambo ya kishujaa pamoja.

Taifa likawatuma wapiganaji wake hawa Zaire kwenye vita. Mizinga, milio ya risasi na vita vinaweza kuleta tatizo la kisaikolojia linaloitwa post traumatic stress au battle fatigue.

Nchi zilizoendelea huwa zinawasaidia mashujaa wake wanaougua battle fatigue kwa matibabu na namna ya kuishi. Inavyoonekana kwetu walipatiwa matibabu kiasi kisha wakafukuzwa jeshini.

Walibidika kujitafutia maisha. Tunaambiwa walilazimika hata kufanya kazi za kupasua kokoto Mtwara. Mungu sio, Athumani, mwalimu wao akapata habari ya kuwepo kwa nafasi ya kazi ya kuwalinda viongozi wa Chadema. Akawakumbuka wanafunzi wake mashujaa wanaosota, akawaunganisha kwenye hiyo fursa.

Chuki zikaanza. Wakatafutiwa makosa.

Naona kwenye picha walivyokonda sana. Bila shaka wamepitia mateso mengi. Kosa lao ni lipi? Walianza kwa kujiunga na jeshi ili wailinde nchi yetu. Shukrani yetu iko wapi?
 
Wanajeshi waliopo kazini wayaone hayo wanaopitia wenzao walivyoteseka
 
The Palm Tree respect Sana
 
Maswali yako..na wayasome akina Mahita na Kingai and Co.. Kutafakari Unyama waliowafanyia watu hawa. Mimi ua natafakari kwani kigezo cha kupata maelezo ya mtu kwann kiwe ni Kutuza utu wa mtu? Hivi kwani ni binadam uwe Na Unyama zaidi ya Wanyama wa Polini? Hivi tabia hizi za kinyama ni mafunzo ya kambini ama Makosa ya malezi kwa wazazi wao?
 
Ni sawa mkuu. Mimi maoni yangu atatoa maamuzi kuipendelea Jamhuri lkn siku hiyohiyo atajiondoa kwenye kesi.
 
Inasikitisha sana, na hao wote waliyofanya huo huonevu watalipa hapa hapa duniani na Alhera

Wewe fikilia shaidi anaapa kwa kutumia jina la m/Mungu kwa kusema uhongo mahakamani kwa lengo na Nia ya kutenda uhovu. Hivi m/Mungu atawaacha salama kweli?? Sijui labda kuwe hakuna mungu
 
Umeongea kitu kizito sana, Mungu akasimame nawe kwenye majonzi.
 
Jaji akiikubali hiyo barua jamuhuri itakuwa na mitiani mkubwa sana maana itabidi wamthibitisha Lingwenya kama alivyoomba

Na ktk kumthibitishia Kuna takiwa kufanyika uchunguzi na ktk uchunguzi Kuna mambo mengi sana yatatakiwa yawekwe wazi. Hapo cha ha ndio patamu

Ninavyoona mimi jaji hawezi kukubali hiyo barua ipokelewe, na sijui ataikataa vipi isipokelewe maana Mmhh..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…