Yaliyonikuta wakati nafuatilia loss report

Mukuu123

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2019
Posts
319
Reaction score
1,223
Habari ndugu zangu,

Yani leo hii nimeachwa apeche alolo kwa utaratibu wa kufuatilia loss report baada ya kupata mafuriko na kuondokewa na baadhi ya vitu vyangu muhimu, so nikajikaza na kasema niende kituoni sasa kufika pale naambiwa niende stationery ya karibu na pale kituoni.

Akili yangu nikajua itakuwa copy tu ya Tsh 100 Au 200 naambiwa eti nitoe 2500, aiseee ghafla nikaishiwa nguvu na kuzimia, ile kuzinduka najikuta niko hospitali na nurses akanambia mitano tena.

Hivi wadau ndio utaratibu huu kweli?
 
loss report siku hizi inapatikana online mkuu jeshi la polisi limekua la kisasa wameishatoka kwenye ujima.
 
Kwa sas tunataka kupeleka meli kubwa ya mizigo chato, ngoja kwnz tumalizie mipango yetu ndo tushugulikie yako.
 
Ndio
 
loss report siku hizi inapatikana online mkuu jeshi la polisi limekua la kisasa wameishatoka kwenye ujima.
Dah mkuu online miyeyusho mara nyingi nafikia hadi kwenye kulipa ukishalipa wanakwambia ripoti yako bado haijathibitishwa na mchezo unakua umeishia hapo
 
Mimi nilipoteza simu, nilivyo report kwenye kampuni ya mtandao wa simu nayotumia nikaambiwa niende police kupata hiyo loss report.

Nikishangaa kufika police ya kawe naelekezwa kibanda cha airtel nje ya police, nilienda nikiwa najua bei ni 500 nikishangaa naambiwa 2000.

Ikiwa policetz wameamua kwenda ki digital iweje hayo yafanywe na mawakala nje ya kituo cha police?,kwanini waendelee kuwa aminisha watu kua loss report ni miatano wakati sio hivyo?.

Nikisema police wanashiriki utapeli nitakosea?
 
loss report siku hizi inapatikana online mkuu jeshi la polisi limekua la kisasa wameishatoka kwenye ujima.
Tatizo ni ulaghai kwa wananchi kua loss report ni 500 wakati garama anayo lipa mwananchi sio hiyo.

Pili, kwanini hayo yafanyike nje ya vituo vya police?,na sio police wenyewe wasiwe na huo mfumo wa malipo palepale ofisini kwao?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…