Yaliyotokea Kenya, yanatafakarisha. Pastor Mackenzie na Pastor Odero wamewashawishi wafuasi wao wafunge bila kula ili eti wakifa wakutane na Yesu

Yaliyotokea Kenya, yanatafakarisha. Pastor Mackenzie na Pastor Odero wamewashawishi wafuasi wao wafunge bila kula ili eti wakifa wakutane na Yesu

kikaniki

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2014
Posts
508
Reaction score
968
Sina nia ya kukebehi imani au dini ya mtu. Lakini lazima itakuwa tumerogwa. Nani AMETUROGA?

Hizi imani vipi? Yaliyotokea Kenya, yanatafakarisha. Pastor Mackenzie na Pastor Odero wamewashawishi wafuasi wao wafunge bila kula ili eti wakifa wakutane na Yesu Kristo. Waumini masikini wakaitikia Naam! Mamia wamekufa. Msitu wa Shakahola umejaa maiti. Kila kukicha wanaokota maiti.

Miaka michache iliyopita nchini Uganda tuliona ya Kibwetere? Waumini takribani mia tisa walidanganywa. Wakajazwa kanisani na kuchomwa moto. Wakafa kijinga kabisa, eti ni safari ya kumuona Yesu Mwokozi.

Tumekuwa tukishuhudia visa na mikasa ya wachungaji na makanisa. Wapo wanaowalisha waumini wao kila takataka (nyoka, mijusi n.k) na wengine kuwanywesha jiki eti ni njia ya kuwatakasa dhidi ya dhambi.

Wapo Wachungaji ambao wakiwa wanaingia Kanisani, waumini hulala kifudifudi ili Mchungaji apite juu ya migongo yao akiwa anaenda madhabahuni.

Wengine (wanawake) wanaambiwa waje na nguo za ndani (chupi) eti ili ziombewe na matatizo yao yataondoka.

Hapa kwetu tunaona wapo wanaouziwa maji yaliyoombewa, chupa ya lita moja Kwa shilingi elfu tano. Maelfu ya katoni za maji yanauzwa na kununuliwa na waumini wajinga na masikini. Nimeshuhudia watu wakiuziwa leso kwa shilingi elfu 5, leso ambayo ukienda dukani ni shilingi mia tano tu.

Wapo wajinga wengine ambao, waliandamana na kuweka kambi airport eti wana wito wa kwenda Jerusalem. Upuuzi.

Wachungaji hawaishi vituko na vibweka kama vya kaboka mchizi. Rafiki yangu mmoja aligombana na mke wake, kisa mke anataka salary slip ya mumewe ili ampelekee Mchungaji akapigiwe percent ya kuwasilisha kanisani kila mwisho wa mwezi.

Miezi michache iliyopita, tulisoma katika magazeti Bwana mmoja ameenda mahakamani kuomba mahakama ikubali kuvunja ndoa ya mume na mke, kisa mke ambaye ni mwalimu ameomba mkopo Benki na mkopo wote kumpa "baba Mchungaji".

NANI AMETUROGA?
 
Shetani anahitaji damu nyingi mno. Mkiwazuia damu wataipata wapi?

Kila mmoja atunze familia yake.

Imani za wageni zimetufanya tuwe wajinga
 
Mkuu umeona mbali sana. Hii hali siku hizi naona inakwenda kasi sana. Kitabu kitakatifu " Biblia" kina sema utowapo sadaka kwa mkono 'say'wa kuume basi hata wa kushoto usitambue kiasa chake; lakini leo, kuna wanao andika kwenye madaftari, wengine kwenye miamara n.k. Hali imebadilika.
 
Kweli tuwe makini sana na wale wanaojiita watumishi wa Mungu, wengi ni wezi na mbwa mwitu wakali.
 
Sina nia ya kukebehi imani au dini ya mtu. Lakini lazima itakuwa tumerogwa. Nani AMETUROGA?
Hakuna kurogwa ni ujinga aliochanganyika na upumbavu ndio chanzo cha matatizo yetu!! viongozi wa nchi za kiafrika ni mafisadi na ndio maana wanauza nchi zao kwa kuingia mikataba bila kuielewa; we finirai tu RASI anasaini mkataba na Wachina uliondikwa kwa lugha ya MANDARIN, ataelelwa kweli nini kilichoandikwa humo? Haya yametokea ana ndio maana Magufuli hata msipompenda alifuta ule mkataba wa kujenga bandari ya Bagamoyo!
 
Huoni kuwa serikali ndio ina mguu hapo?
Haiwezekani wakijua kabisa kuna matapeli ambao ingawa wanagawana wapumbavu baina ya Chama na Dini zao hizo
Lakini bado wanawaacha wazidi kuwa wapumbavu kila kukicha maana kuna misukule mingine huwa inadanganywa hivyo hivyo kwa Kanga na kofia

Wala siwezi Sema tumerogwa ila ni ujinga tu na utumwa bado umewajaa watu vichwani, haiwezekani Serikali inakaa kimya tu wakiona dhahiri watu wanapotea

Mbona Kagame kashinda huu upumbavu ingawa nae ni mkristo ila aliona kuna ujinga mwingi unafanyika na wafuasi wanatoa hela zao kidogo kwa kuwapa hao majizi
 
Back
Top Bottom