Yamemkuta, anaomba ushauri


Kwa mujibu wa jirani yangu hii ni mara ya kwanza kuziona sms hizo hii ni kutokana na kutokuwa na mazoea ya kusoma sms kwenye simu ya mumewe. Ila sms zinaonyesha walianza mahusiano muda mrefu. Jirani kaamua kutafuta nyumba apange sehemu nyingine kwani anasema hana imani naye tena. Anadai hivi karibuni mumewe amekuwa akinuna mara kwa mara na kumkaripia hata kwa kosa dogo analolifanya tofauti na mwanzo. Mumewe anadai walikuwa tu wanachati na huyo dada sio mpenzi wake.
 
Msaidie vizuri jirani yako.... atumie akili zake badala ya akili za kuambiwa. Anapoamua kuondoka ndio talaka au anataka apumzike kidogo? Kama ni talaka ahakikishe amefuata taratibu zote.... awaone viongozi wa dini waongee na mumewe, then wote wawili, kisha kama bado kuna haja ya kutengana aende mahakamani kuomba talaka kulingana na sheria ya ndoa ya mwaka 1971.
Mwambie pia akumbuke kuna mambo ya msingi wanayopaswa kuweka sawa kabla ya kuetngana kama matunzo ya mtoto/watoto, kugawana mali walizopata pamoja, madeni waliyokopa pamoja n.k japo mimi binafsi naamini talaka ni hatua ya mbali sana. SIDHANI KAMA AKIONYWA NA WATU WENYE BUSARA HAPO MTAANI KWENU AU VIONGOZI WA DINI KAMA ATAREJEA. Nashauri jirani yako afikiri mara mbili kama kujitoa kwenye ndoa ni nafuu zaidi kuliko kubaki na kama yupo tayari kukabiliana na mtu asiyemjua kuwa mumewe n.k Mwisho "akili za kuambiwa hapa JF, achanganye na za kwake"
 
Amwambie mumewe ampe kama alivyompa hawala yake cha mtoto.... halafu na kikubwa chake akishindwa ndio zogo lianze..
 
yeye arudi tuu kwa mume wake...wanaune kuwa na hawara ni kitu normal sana so ataakienda kwa mwengine atakutana na hayo hayo. so ataolewa mara ngapi??. apotezee tuu na ajue kuwa siku hizi haupo peke yako. kama vipi nae akipata maujanja aonje onje mihogo mingine.
 
Of coz alikosea kuperuzi simu ya mumewe, ajaribu kufikiri asije akawa ndo chanzo cha jamaa kutoka nje, wayazungumze wao kwanza lakini kuachana sio dawa. Matatizo ya uhusiano huwa hayatatuliwi kwa kuachana ila kuachana ni njia ya kuyaepuka incase yakizidi.
 
aisee mpe pole sana ila hii tabia ya wana jf kutoa visa vyao kwa kusingizia wengine inaniuz,kwan ukisema ni wewe utakuwaje?a'way,ajitahidi kuyamaliza 2 na mumewe na huyo ameumia mpaka kuchukua uamuz wa kuondoka inaelekea yeye alikuwa hachakachui,kwahiyo arudi kwa mumewe na yeye akili iwe kichwani mwake.
 
Huyo jamaa ake anafanya kwa siri pia kwa tahadhari, kwa kuwa anamheshimu mkewe,
huyo mke akiona sawa amuache mmewe ili akakutane na ambao watamuomba tigo, huku wakirudi home usiku wa manane wakinukia marashi ya kike, au wakienda live na mahawara zao,
 



Mh! kwa stail hii hakuna atakayepona. Eee Mungu tusaidie. Ujumbe umefika nashukuru
 
Amwambie mumewe ampe kama alivyompa hawala yake cha mtoto.... halafu na kikubwa chake akishindwa ndio zogo lianze..

Hiyo nzuri imetulia. Mahawala wanajua kusifia hata kama siku hiyo hakuridhika atamsifia ili amteke jamaa.
 


Duh! kumbe ya jirani yangu ni cha mtoto.
 
Hizo ndio changamoto za ndoa! Mwambie, akaze buti kuhakikisha kwamba kiu, nguvu na ufundi wa mumewe anautumia ipasavyo na kuzimaliza kabisa siyo kujidekeza na kusema amechoka. Mwanamke kujituma! pigania nafasi yako kwa AKILI.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…