Yamenikuta naombeni ushauri, biashara yangu haiendi vizuri

Yamenikuta naombeni ushauri, biashara yangu haiendi vizuri

proxy

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2016
Posts
1,479
Reaction score
1,348
Habari wana JF wenzangu,

Mimi ni mjasiriamali takribani miaka kadhaa sasa, nafanya biashara ya stationaries na biashara zingine zinazolingana na hiyo hapo juu.

Lengo la kuandika Uzi huu ni kuomba ushauri kwa takribani miaka 3 hii ya karibuni biashara haifanyi vizuri mpaka imefikia point pesa za kulipa pango natoa kutoka vyanzo vingine vya pesa.

Kwa sasa nina mfanyakazi mmoja ila bado mambo yanazidi kuwa magumu siku hadi siku, kinachopatikana baada ya kutoa gharama kama vile umeme, mshahara wa mfanyakazi, pango, ulinzi ni kidogo sana na Mara nyingine hata faida hamna kabisa.

Naomba ushauri wenu nini niweze kufanya ili kujinasua na hili janga maana bado ni nia ya dhani ya kuendelea na biashara.
 
Waganga wa kienyeji wanapiga hela ndefu kwa mujibu wa utafiti.
Jiunge nao.
 
Panua huduma,wwateja wataongezeka.Sajiri biashara yako BRELA, kisha GPSA.Ongea na wakuu wa shule na walimu wakuu wa shule za msingi.pia tafuta wakuu wengine wa taasisi za selikali ili uwe supplier wao.kwa njia hii utakuwa umepata wateja wapya.
 
Kwa uelewa wangu mdogo wa biashara, biashara ya stationery na nyumba ya kupanga ukiviweka karibu na university upatapa tu wateja. Fanya urafiki na maofisa wa serikalini kama unaweza kupata tenda ya kupeleka stationery ya vikao vya ofisi.
 
HAKUNA timu ya soka inayoweza kuwa IMARA bila kununua na kuuza wachezaji. Hata Katika biashara kanuni hiyo ni muhimu. Biashara Ukiona hailipi sio vibaya kuiuza.
 
Ninachokiona kila mtu anatoa tu hisia zake...
kiukweli ulitakiwa kuelezea mfumo wa biashara yako kabla ya miaka mitatu.... je,wakati unapata faida na kipindi hiki ambacho hupati faida kuna utofauti gani yaani unadhani ni kwa nini biashara imeshuka

Nadhani hicho ndo cha muhimu ili uwasaidie wadau kujua tatizo ni aidha la ndani ama la nje ya uwezo wako... hii itakusaidia kujua aidha ni vyema kufanya maboresho ama kubadilisha biashara
 
pole sana mie nilitaka kufanya hii biashara,unanitisha mkuu,lol,ni ngoja ni ku PM,lol
 
Cha kwanza mshukuru Mungu kwa kuwa malaika wake wanakupigania na u mzima wa afya,pili nipende nikushauri hebu jaribu kutafuta vitu ambavyo nitofauti vya kibiasha kama huduma za kifedha na uanze kuzifanya,tatu hebu jaribu kuzungunza kwenye ofisi kama yako nauone kuna Huduma gani wanazo zifanya wenzako nawe ufikirie kwa namna iliyo bora zaidi na uzifanye,asante.
 
Nashukuru Sana kwa michango yenu nduguzangu, kikubwa ni kwamba hamna chochote kilichotokea ofisin zaidi ya biashara kuanza kudroup tu, cha msingi nitajitahidi kuendelea kupambana vyovyote iwezekanavyo maana haya maisha si ya kubweteka.
 
Nashukuru Sana kwa michango yenu nduguzangu, kikubwa ni kwamba hamna chochote kilichotokea ofisin zaidi ya biashara kuanza kudroup tu, cha msingi nitajitahidi kuendelea kupambana vyovyote iwezekanavyo maana haya maisha si ya kubweteka.
Tatizo haujipi muda wa kutosha kuichunguza sababu na haujaipa uziti... ndugu vita utakayoingia ni ya kupigana na tatizo lisilojulikana hivyo kama unadhani ni kheri bhasi na uendelee
 
Habari wana Jf wenzangu,

Mimi ni mjasiliamali takribani miaka kadhaa Sasa, nafanya biashara ya stationaries na Biashara zingine zinazolingana na hiyo hapo juu,

Lengo la kuandika Uzi huu ni kuomba ushauri kwa takribani miaka 3 hii ya karibuni biashara haifanyi vizuri mpaka imefikia point pesa za kulipa pango natoa kutoka vyanzo vingine vya pesa,

Kwa Sasa nina mfanyakazi mmoja ila bado mambo yanazidi Kuwa magumu siku hadi siku, Kinachopatikana baada ya kutoa gharama kama vile umeme, mshahara wa mfanyakazi, pango, ulinzi ni kidogo Sana na Mara nyingine Hata faida hamna kabisa.

Kwa minaajili hii naomba ushauri wenu nini niweze kufanya ili kujinasua na hili janga maana bado ni nia ya dhani ya kuendelea na biashara.
Pole
 
Endelea kumnyoosha magu mkuu. Yeye si kasema July wanabaki vipanga mjini, sasa we komaa naye prove him wrong!
 
Biashara ya Stationery zimeasiriwa na utandawazi, zamani mwanafunzi anaenda kutoa kopi kitabu cha page 290. Sasa ivi kitabu icho anaweka katika Tablets au Simu yake anakula maisha, na mavyuoni walimu assignments wanakusnya katika email [emoji391] address na kusaiisha.
Ndio maana biashara za stationery zimeangukia pua sana
 
Back
Top Bottom