Yamoussoukro: Ivory Coast's abandoned Capital

Niliwahi kukusanya video hizi na picha za miji na majumba yaliyojengwa na viongozi halafu yakabaki magofu baada ya uongozi wao kuisha. Ukiacha miji hii ya Yamoussoukro na Gbadolite kuna majumba mengi ya kifahari yaliyoachwa na viongozi ambayo sasa ni magofu.

Palaces nyingi za Saddam Hussesin zilizokuwa kaskazini mwa Iraki zimebaki magofu tu; zilizopona ni zile zilizokuwa
Baghdad, lakini zile za kaskazini zote hazipo tena.



Palace ya Mfalme haile Serrassie leo hii ni gofu; ndani ya jumba hili ndimo Ojukwu na Gowon walijaribu kupatanishwa kumaliza vita ya Biafra bila mafanikio.


Lodge ya Idi Amin huko Pakuba leo hii ni gofu. Amini alikuwa akija kupumzika hapa na mmoja wa wake zake karibu kila wikiend kwa helicopter.


Palace ya Mfalme Bokassa leo hii ni gofu

 
Ila unaambiwa alitumia zaidi ya €300 mln kujenga Yamoussoukro, huyu na Mobutu ndio walewale! nadhani ndo maana Bunge likapitisha sheria ya kuitamka Dodoma makao makuu ya nchi ili asije akatokea kiongozi mwingine akapinga! Ila nadhani watu wana-exaggerate sana ujenzi wa Chato Airport! Maana mpango ni kila mkoa kuwa na Uwanja wa size ile!
 
Ujenzi wa uwanja chato haukuwa sawa na si kuexaggerate mambo. Huwezi jenga uwanja wenye vipimo vya uwanja wa kimataifa kijijini. Jambo lile halina tofauti na waliyofanya Mobutu na Bokassa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…