Yanayojiri kwenye Sakata la Mwalimu kumchapa kikatili Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Wilayani Kyerwa, Kagera

Yanayojiri kwenye Sakata la Mwalimu kumchapa kikatili Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Wilayani Kyerwa, Kagera

paul miteda

Senior Member
Joined
Jan 19, 2023
Posts
131
Reaction score
588
Tafadhali ni nani anayejua hii shule?

====

UPDATES: 1
Kwa mujibu wa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na wenye Mahitaji Maalumu Dorothy Gwajima, Serikali imefanya ufuatiliaji wa kina na kubaini kuwa tukio hili lilitokea Januari 10, 2023 kwenye Shule moja ya Msingi iliyopo Wilayani Kyerwa, Kagera.

Akithibitisha hayo kupitia Akaunti yake rasmi ya Mtandao wa Instagram, Waziri Gwajima amesema kuwa hali ipo kwenye udhibiti mzuri (Situation is under control) na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Albert Chalamila atatoa taarifa inayohusu tukio hilo Januari 25, 2023.

Waziri Gwajima amelaani tukio hilo na amewaasa walimu kuzingatia utaratibu wa adhabu wanazotoa kwa wanafunzi, pia amewataka kuheshimu sheria kwani Hatua kali zitachukuliwa kwa wale watakaofanya aina hii ya ukatili.





UPDATES: 2
Mwalimu aliyeonekana akimuadhibu mwanafunzi kinyume na taratibu, akimchapa kwenye nyayo za miguu, amesimamishwa na kutenguliwa Kwa nafasi yake kama Mwalimu mkuu. Pia, ameshaandikiwa Mashtaka kwa Mamlaka ya TSC ili akajibu tuhuma zinazomkabili.

Waziri wa Elimu, Profesa Adolf Mkenda amesema hatua stahiki zitachukuliwa dhidi ya mwalimu huyo.

UPDATES: 3

68E8BB3B-6F68-4897-84AA-28240A8DF904.jpeg

Mtuhumiwa yupo ndani, Mkuu wa Mkoa ameshafika hospitalini kumuona mtoto na Jeshi la Polisi linaendelea na hatua zake.
 
so sad
unakuta mwalimu katoka kuachana na mumewe alafu ahsubui anaingia ofisini
whata do you expecting

ila hata kama unastress vipi huwezi kumfanyia hivo mtoto wa mwenzio !!!
 watu kama hawa inatakiwa ndo wawe wa kuwafanyia mfano ili kenge wengine wenye tabia kama hizi wasijitokeze
 
Sasa mtoto kama huyo atakuwa amefanya kosa gani mpaka anapewa adhabu kama hiyo kisa kapata 1/10 au
Na pembeni kule wamekaa wengine wanacheka tu kama ni jambo la kawaida linalotendeka 🚮 kuna watu ni matakataka
Hv Mwalimu ukikausha ukawa unafundisha zako ukimaliza unaendelea na mishe zako utapungua nini?
 
so sad
unakuta mwalimu katoka kuachana na mumewe alafu ahsubui anaingia ofisini
whata do you expecting

ila hata kama unastress vipi huwezi kumfanyia hivo mtoto wa mwenzio !!!
 watu kama hawa inatakiwa ndo wawe wa kuwafanyia mfano ili kenge wengine wenye tabia kama hizi wasijitokeze
Ni unyama huyu atafutwe aliko
 
Ebu mfutilieni mwalimu YUSUPHU PANGOMA na mwenzie mmoja kama ana mguu mbovu anatembea na gongo la chuma ni walimu wa kuigwa wanaishi poa sio hao washamba wakishavaa hayo maviatu makubwa wanakanyanga mwanafunzi kama anataka kuchinja mbuzi.

Mwalimu PANGOMA na mwenzio yule mweny mguu mbovu watu safi kabisa wanajielewa huko Mara wanafunzi wanawapenda sana na wamekuwa msaada mkubwa sana kweny jamii zao..Sio huyo anataka kuogopewa ni ushamba.
 
Daah aisee yàaani kiukweli ndugu zetu walimu nyie nadhani miongoni mwenu kuna baadhi yenu ni vichaa ka.a si kurogwa kabisa asee

Maana kwa mtu mwenye akili zake timamu hawezi kufanya ukatili na ujinga kama huu yaani mwanaume mwenye akili timamu unawezaje kumfanyia mtoto unyama na ukatili wa kiwango hiki tena mtoto mdogo kabisa ambaye daah ata sijui kakosa nini lakini mmmh

Nadhani serikali inapaswa kufanyanya juhudi nyingi sana hasa za kisaikolojia ya hawa wenzetu walimu ili wawe timamu kichwani asee.

Kiukweli inasikitisha sana mpaka nimeshindwa ata kuiweka apa iyo video alafu cha ajabu kabisa yaani walimu wenzake na uyo mwalimu anayefanya unyama wako wanamwangalia tu mwenzao na kufurahia unyama anaoufanya daah ama kweli.View attachment 2494438View attachment 2494439
Screenshot_20230124-215148_WhatsApp.jpg
 
Back
Top Bottom