LGE2024 Yanayojiri kwenye Uzinduzi wa Ilani ya ACT Wazalendo kuelekea Uchaguzi Serikali za Mitaa 2024

LGE2024 Yanayojiri kwenye Uzinduzi wa Ilani ya ACT Wazalendo kuelekea Uchaguzi Serikali za Mitaa 2024

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760


PICHA NA MATUKIO YA UZINDUZI WA ILANI YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, VIJIJI NA VITONGOJI
20241117_112944.jpg
20241117_112939.jpg
Huu ni Ukumbi wa Hakainde Hichilema; upo katika Jengo la Maalim Seif Magomeni Dar es salaam. Hapa ndipo ambapo Ilani ya ACT Wazalendo itazinduliwa.

Mgeni rasmi ni Kiongozi wa Chama Semu Dorothy

====

Semu Dorothy; "Leo tunazindua ilani. Kwa hivyo ni siku ya kihistoria katika nchi yetu; siku ambayo inaweka utamaduni mpya wa kisiasa katika kuendea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji. Uchaguzi huu hatuendi kuukabili kwa maneno matupu."

Snapinsta.app_466895725_557040680382082_4560464882601781531_n_1080.jpg

Snapinsta.app_466693181_1639633686989200_6337611841899124658_n_1080.jpg

Snapinsta.app_466605071_853547953338464_310601909015583354_n_1080.jpg

Snapinsta.app_466597716_558965870176384_2225178045155242450_n_1080.jpg
20241117_135259.jpg
20241117_135256.jpg
20241117_135253.jpg
20241117_135250.jpg

Kiongozi wa ACT Wazalendo, Ndugu Semu Dorothy akizindua Ilani ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji.

Ilani hiyo imezinduliwa leo Novemba 17, 2024 katika Ukumbi wa Hakainde Hichilema Makao Makuu ya ACT Wazalendo Magomeni Dar es salaam.

"CHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza kusikitishwa na mwenendo wa usikilizwaji wa rufani za wagombea ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa.

Mchengerwa aliagiza utekelezaji wa agizo kufanyika kwa mapitio ya kuenguliwa kwa wagombea.

Kupitia taarifa ya chama hicho iliyotolewa na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Isihaka Mchinjita, amesema tathmini waliyofanya imebaini kamati za rufani zimeendelea kuwaengua wagombea wao.

Amesema hata pale ambapo makosa yaliyojitokeza yalikuwa madogo, hayapaswi kuathiri mchakato wa uchaguzi.

Mchinjita amesema wagombea wao kutoka majimbo mbalimbali, yakiwamo Tandahimba (500) Newala Vijijini (93), Kinondoni (80) na Bukoba Vijijini (621) wameenguliwa licha ya maelekezo yaliyotolewa na Waziri Mchengerwa, yanayotaka kuzingatia haki na kuepuka kuadhibu makosa madogo yaliyojitokeza.

Mchinjita amesema chama hicho kinalaani ucheleweshaji na kutochukuliwa hatua stahiki kwa wasimamizi wa uchaguzi katika maeneo mengi kwa kushindwa kufanyia kazi maelekezo ya kuwasilisha fomu za uteuzi ili kufanya marekebisho kwa wagombea walioenguliwa.

Kutokana na hali hiyo, amesema wanamwomba waziri mwenye dhamana kusimamia utekelezaji wa agizo lake kwa kuhakikisha haki inatendeka.

“Tutamwandikia waziri orodha ya maeneo ambayo agizo lake halijatekelezwa kikamilifu pamoja na vielelezo husika.


“Tutachukua hatua za kisheria zikiwamo kufungua kesi mahakamani kupinga uamuzi wa kuwaengua wagombea wetu ili kuhakikisha uchaguzi unarudiwa katika maeneo husika,” amesema.

BONYEZA HAPA KUSOMA ILANI YA ACT WAZALENDO 2024 SERIKALI ZA MITAA
 

Attachments

Acha tuone kitachojiri ktk mkutano. Wengine tumeshaachana na mambo ya vyama na siasa maana ni utoto na ujinga mwingi.
 


PICHA NA MATUKIO YA UZINDUZI WA ILANI YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, VIJIJI NA VITONGOJI
Huu ni Ukumbi wa Hakainde Hichilema; upo katika Jengo la Maalim Seif Magomeni Dar es salaam. Hapa ndipo ambapo Ilani ya ACT Wazalendo itazinduliwa.

Mgeni rasmi ni Kiongozi wa Chama Semu Dorothy

Safi sana Act wazalendo hiki ndio chama mbadala au chama mtambuka inapendeza !
 


PICHA NA MATUKIO YA UZINDUZI WA ILANI YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, VIJIJI NA VITONGOJI
Huu ni Ukumbi wa Hakainde Hichilema; upo katika Jengo la Maalim Seif Magomeni Dar es salaam. Hapa ndipo ambapo Ilani ya ACT Wazalendo itazinduliwa.

Mgeni rasmi ni Kiongozi wa Chama Semu Dorothy

====

Semu Dorothy; "Leo tunazindua ilani. Kwa hivyo ni siku ya kihistoria katika nchi yetu; siku ambayo inaweka utamaduni mpya wa kisiasa katika kuendea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji. Uchaguzi huu hatuendi kuukabili kwa maneno matupu."

View attachment 3154508View attachment 3154507View attachment 3154506View attachment 3154505
Kiongozi wa ACT Wazalendo, Ndugu Semu Dorothy akizindua Ilani ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji.

Ilani hiyo imezinduliwa leo Novemba 17, 2024 katika Ukumbi wa Hakainde Hichilema Makao Makuu ya ACT Wazalendo Magomeni Dar es salaam.

"Chama cha ACT Wazalendo kitaendelea na kampeni kabambe kwenye maeneo ambayo wagombea wetu wameteuliwa. Chama kimejiandaa kwa kampeni ya kishindo na ya kisayansi kuhakikisha kinapata ushindi kwenye mitaa, vijiji na vitongoji vyote ambavyo tuna wagombea. Kwa kuanzia, kesho tarehe 17 Novemba 2024, Chama cha ACT Wazalendo kitazindua Ilani ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji itakayotoa mwongozo wa kisera kwa wagombea wetu"- Mchinjita

Taarifa ya Makamu Mwenyekiti wa chama cha ACT Wazalendo bara, Isihaka Rashidi Mchinjita iliyotolewa tarehe 16 Novemba 2024.

Wanazindua ilani wakati wagombea wao wote wameondolewa hawa ACT mbona Kama wanavichaa ?
 
Back
Top Bottom