Albinoomweusi
JF-Expert Member
- Oct 28, 2016
- 3,433
- 8,585
.
Swali langu la kwanza ni, lengo mama kabisa msimu huu lilikuwa ni lipi?? Najua jibu litakuwa, 'Kutwaa ubingwa wa ligi kuu na kupata nafasi ya kushiriki klabu bingwa mashindano yajayo'
Swali la pili litakuwa, 'Mikakati gani iliwekwa kuhakikisha lengo mama linafikiwa?' Naweza nisiwe na jibu sahihi lakini naweza kubuni, marekebisho muhimu yalifanywa kikosini, kuanzia kwa wachezaji hadi kwenye benchi la ufundi.
Hili jibu linaweza kuzua maswali mengine yatakayokuwa vipengele vya swali la pili. Mosi, Wachezaji waliokuja, je ni kweli wana uwezo wa kukupa ubingwa?? Pili, Je wanaendana na falsafa ya timu?? Tatu, una hakika watazoeana ndani ya muda ambao watakuwa tayari kukupa ubingwa??
Tuseme hayo yote majibu yake ni ndiyo. Swali langu lingine linakuja, Umewatazama wapinzani wako wa karibu na kujiaminisha kuwa unaweza kuwashinda kwenye vita ya ubingwa??
Tuseme nitajibiwa tena, NDIYO. Nitaguna halafu nitauliza, Mmeitazama Simba lakini?? Kumbuka pale juu nimesema 'kwa uelewa wangu mdogo'. Najua mnafahamu kuliko mimi.
Hapo nitaulizwa, Je naandika haya kwasababu Yanga amefungwa kwa mara ya kwanza?? Nitajibu Hapana! Kufungwa siyo dhambi. Je kufungwa na Coastal kunaweza kuwatoa Yanga kwenye mbio za ubingwa?? Nitajibu Ndiyo. Ndiyo kama watachagua kuyaishi haya matokeo, ndiyo kama watashindwa kupata majibu ya kwanini hawafanyi vizuri??
Swali langu la mwisho litakuwa, Je Yanga Afrika mnapaswa kuumia kama mtakosa ubingwa mwisho wa msimu?? Nitawasaidia kujibu, Hapana. Kwanini?? Kwasababu ya majibu ya maswali niliyouliza kabla.
Si rahisi kuchukua ubingwa katika mazingira waliyopo Yanga msimu huu, nasisitiza Sijasema HAIWEZEKANI, nimesema, SI RAHISI. Ugeni mwingi kikosini, aina ya wachezaji na Nature ya Simba ambaye ndiye mpinzani wa karibu, ndiyo sababu zangu.
Nadhani ni vema, Yanga ikatulia na kujipanga zaidi badala ya ku'panic' kwa kupoteza rekodi ya 'Unbeatean' au kama itakosa ubingwa mwisho wa msimu. Tukumbuke Tanzania tunaweza kuingiza timu nne mashindano ya Afrika msimu ujao. Kama hili litatokea, bado Yanga watakuwa hawajapoteza lengo mama.
Napokea maoni 'BILA MATUSI'[emoji120].
Swali langu la kwanza ni, lengo mama kabisa msimu huu lilikuwa ni lipi?? Najua jibu litakuwa, 'Kutwaa ubingwa wa ligi kuu na kupata nafasi ya kushiriki klabu bingwa mashindano yajayo'
Swali la pili litakuwa, 'Mikakati gani iliwekwa kuhakikisha lengo mama linafikiwa?' Naweza nisiwe na jibu sahihi lakini naweza kubuni, marekebisho muhimu yalifanywa kikosini, kuanzia kwa wachezaji hadi kwenye benchi la ufundi.
Hili jibu linaweza kuzua maswali mengine yatakayokuwa vipengele vya swali la pili. Mosi, Wachezaji waliokuja, je ni kweli wana uwezo wa kukupa ubingwa?? Pili, Je wanaendana na falsafa ya timu?? Tatu, una hakika watazoeana ndani ya muda ambao watakuwa tayari kukupa ubingwa??
Tuseme hayo yote majibu yake ni ndiyo. Swali langu lingine linakuja, Umewatazama wapinzani wako wa karibu na kujiaminisha kuwa unaweza kuwashinda kwenye vita ya ubingwa??
Tuseme nitajibiwa tena, NDIYO. Nitaguna halafu nitauliza, Mmeitazama Simba lakini?? Kumbuka pale juu nimesema 'kwa uelewa wangu mdogo'. Najua mnafahamu kuliko mimi.
Hapo nitaulizwa, Je naandika haya kwasababu Yanga amefungwa kwa mara ya kwanza?? Nitajibu Hapana! Kufungwa siyo dhambi. Je kufungwa na Coastal kunaweza kuwatoa Yanga kwenye mbio za ubingwa?? Nitajibu Ndiyo. Ndiyo kama watachagua kuyaishi haya matokeo, ndiyo kama watashindwa kupata majibu ya kwanini hawafanyi vizuri??
Swali langu la mwisho litakuwa, Je Yanga Afrika mnapaswa kuumia kama mtakosa ubingwa mwisho wa msimu?? Nitawasaidia kujibu, Hapana. Kwanini?? Kwasababu ya majibu ya maswali niliyouliza kabla.
Si rahisi kuchukua ubingwa katika mazingira waliyopo Yanga msimu huu, nasisitiza Sijasema HAIWEZEKANI, nimesema, SI RAHISI. Ugeni mwingi kikosini, aina ya wachezaji na Nature ya Simba ambaye ndiye mpinzani wa karibu, ndiyo sababu zangu.
Nadhani ni vema, Yanga ikatulia na kujipanga zaidi badala ya ku'panic' kwa kupoteza rekodi ya 'Unbeatean' au kama itakosa ubingwa mwisho wa msimu. Tukumbuke Tanzania tunaweza kuingiza timu nne mashindano ya Afrika msimu ujao. Kama hili litatokea, bado Yanga watakuwa hawajapoteza lengo mama.
Napokea maoni 'BILA MATUSI'[emoji120].