Yanga anzeni kuuza tiketi sasa hivi.

man dunga

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2013
Posts
3,358
Reaction score
5,783
Yanga washataja viingilio vya mechi yao ya kombe la shirikisho ambapo kiwango cha chini kabisa ni shilingi elfu kumi.

Sasa ukiangalia viwango vya viingilio inaonesha yanga wanahitaji sana pesa kwa hiyo nawashauri watangaze kwa nguvu hapo mwanza na waanze kuuza tiketi sasa kuliko kusubiria siku ya mechi au siku moja kabla maana kipindi hiki kuna mvua. Ni heri mtu anunue tiketi sasa na siku ya mechi asipokuja sababu ya mvua au nyingine atajijua yeye, lakini siku ya mechi kama ndio siku ya kuuza tiketi na kuna mvua mtakosa pesa na mashabiki.
 
Wazo zuri
 
Vyura wangekua nazo kichwani si wangefanyia kazi mawazo mazuri kama haya
 
Sasa si watazichakachua! Unawafahamu vizuri wabongo lakini? Huwa hawashindwi kitu. Labda kama huo uwanja ungekua umekwisha unganishwa kwenye ule mfumo wa kielektroniki.
 
Nadhani ni mapema, lakini pia wasichelewe, kuanzia mapema wiki ijayo ticket zianze kuuzwa. Mleta Uzi asante sana kwa Ku tu alaert
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…