Mwenye update karibu hapa
----------
Mshambuliaji Donald Ngoma ameifichia aibu timu yake ya Yanga baada ya kusawazisha bao dakika za majeruhi ugenini dhidi ya Majimaji katika mchezo wa ligi uliopigwa kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea.
Ngoma alifunga bao hilo dakika ya 79 kwa kichwa akimalizia mpira wa krosi uliochongwa na Obrey Chirwa upande wa kulia huku ukimuacha mlango Andrew Ntalla asiwe na la kufanya.
Wenyeji Majimaji walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Peter Mapunda dakika ya 54 baada ya kupokea pasi ya Marcel Boniventure aliyoipitisha katikati ya walinzi wa Yanga.
Yanga wameambulia alama nne katika mechi mbili za nyanda za juu Kusini kufuatia sare ya leo na ushindi wa bao moja walioupata dhidi ya Njombe Mji wikiendi iliyopita.
Winga wa Yanga Emmanuel Martin alishindwa kuendelea na mchezo muda mfupi baada ya kuingia kuchukua nafasi ya Geofrey Mwashiuya kipindi cha pili baada ya kugongwa na mchezaji wa Majimaji wakati mechi hiyo ikielekea ukingoni.
Yanga wanarejea jijini Dar es Salaam wakiwa na pointi tano baada ya kucheza mechi tatu wakishinda moja na kupata sare michezo miwili.
CHANZO: Yetu
----------
Mshambuliaji Donald Ngoma ameifichia aibu timu yake ya Yanga baada ya kusawazisha bao dakika za majeruhi ugenini dhidi ya Majimaji katika mchezo wa ligi uliopigwa kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea.
Ngoma alifunga bao hilo dakika ya 79 kwa kichwa akimalizia mpira wa krosi uliochongwa na Obrey Chirwa upande wa kulia huku ukimuacha mlango Andrew Ntalla asiwe na la kufanya.
Wenyeji Majimaji walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Peter Mapunda dakika ya 54 baada ya kupokea pasi ya Marcel Boniventure aliyoipitisha katikati ya walinzi wa Yanga.
Yanga wameambulia alama nne katika mechi mbili za nyanda za juu Kusini kufuatia sare ya leo na ushindi wa bao moja walioupata dhidi ya Njombe Mji wikiendi iliyopita.
Winga wa Yanga Emmanuel Martin alishindwa kuendelea na mchezo muda mfupi baada ya kuingia kuchukua nafasi ya Geofrey Mwashiuya kipindi cha pili baada ya kugongwa na mchezaji wa Majimaji wakati mechi hiyo ikielekea ukingoni.
Yanga wanarejea jijini Dar es Salaam wakiwa na pointi tano baada ya kucheza mechi tatu wakishinda moja na kupata sare michezo miwili.
CHANZO: Yetu