Kwanza nianze kwa kusema kuwa mimi ni shabiki kindakindaki wa Yanga, japo miaka miwili iliyopita nilijipa likizo ya kutoifuatilia. Hili la kutoifatilia ilitokana na timu yangu hii kuwa na mambo mengi ya kuudhi, japo ilipokuwa yafanya vibaya, niliumia.
Msimu huu mpya ulianza kwa tambo nyingi sana. Wakati wa usajili nilikaa kimya kuona hii pendwa itawaleta nani. Wengi waliokiwa wanasajiliwa niliwapa tahadhari, kwani najua mpira wa Tanzania una mengi. Lakini baada ya mechi ya leo niwe muwazi na kuiweka furaha yangu hadharani.
Hakika waliofanya usajili safari hii wametuletea watu kweli kweli. Kuanza kwa Zawadi Mauya, mpaka kule mbele hakika kazi hii ilifanyika kwa kuzingatia Yanga inataka nini kwani mpaka benchi la akiba wamekaa wanaume kweli kweli. Niwaambie mashabiki na wapenzi wa Yanga, timu hii tunatakiwa tuipe muda, itafanya makubwa sana, hasa mwalimu atakapowaelewa wachezaji wake. Pia naomba viongozi watulie, wasiwe na maneno mengi kuingilia benchi la ufundi. Yanga hii naitabiria makubwa sana.
Daima mbele, nyuma mwiko.
Asante timu nzima iliyofanya usajili yanga
Wasalaaam
Msimu huu mpya ulianza kwa tambo nyingi sana. Wakati wa usajili nilikaa kimya kuona hii pendwa itawaleta nani. Wengi waliokiwa wanasajiliwa niliwapa tahadhari, kwani najua mpira wa Tanzania una mengi. Lakini baada ya mechi ya leo niwe muwazi na kuiweka furaha yangu hadharani.
Hakika waliofanya usajili safari hii wametuletea watu kweli kweli. Kuanza kwa Zawadi Mauya, mpaka kule mbele hakika kazi hii ilifanyika kwa kuzingatia Yanga inataka nini kwani mpaka benchi la akiba wamekaa wanaume kweli kweli. Niwaambie mashabiki na wapenzi wa Yanga, timu hii tunatakiwa tuipe muda, itafanya makubwa sana, hasa mwalimu atakapowaelewa wachezaji wake. Pia naomba viongozi watulie, wasiwe na maneno mengi kuingilia benchi la ufundi. Yanga hii naitabiria makubwa sana.
Daima mbele, nyuma mwiko.
Asante timu nzima iliyofanya usajili yanga
Wasalaaam