Yanga Imekubaliana na aliyekuwa mchezaji wake Juma Balinya kuvunja mkataba

Kwa jinsi uchumi wao yanga ulivyo ningekuwa kiongozi nisinge hangaika na wachezaji wa kimataifa, mtu ukitulia wachezaji wazuri wapo hapa hapa bongo wanaoweza kuvumilia. Huwezi kumtoa mtu nchini kwake then usimlipe mshahara miezi 3.
 
Eti mashabiki wa simba wanatoa pole! Tayari wamesha sahau ni miaka michache tu walikuwa katika hali kama wanayopitia Yanga.

Sisi tulimtegemea Manji na ninyi mnamtegemea Mo! Akitoka leo hii huyo Mo wenu kwenye timu, na ninyi mtarudi kule kule! Jambo la msingi ni kuhakikisha timu zetu zinabadili mifumo yao ya kiuendashaji. Zianze kujiendesha sasa kisasa na kama taasisi! badala ya kumtegemea mtu mmoja.

Simba mmeanza na Yanga tutafuata. Huu ni wakati wa mpito tu kama mliopitia nyinyi miaka michache iliyopita kiasi cha kuifanya Yanga kuchukua ubingwa wa ligi kuu kwa mara tatu mfululizo.
 
Wewe unashangaza. Kuna kosa mtu kutoa pole kwa magumu tunayokutananayo? Sasa ulitaka watusodoe? Uungwana ni kupeana pole. Wakati mwingine sisi tunapenda sana wenyewe kunenwa vibaya kwa mitazamo kama yako.

Angalau man enough ya hapo chini umeongea jambo la maana kidogo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yanga ilitiwa GUNDU na changizo la ccm
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…