Yanga imetoa wapi uhalali wa Uhalali wa Kutumia Rangi nyekundu katika Mkataba wao na LaLiga?

Singidan

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2015
Posts
881
Reaction score
942
Anahoji Mwandishi wa habari za michezo Ndg. Saleh Jembe;

Nimezungumza mara nyingi sana kuhusiana na hili suala lakini WASIO NA HOJA wakaishia kwenye Matusi, sasa leo TUJIFUNZE TENA

ANGALIA LOGO ya @sevillafc ina rangi nyingi nyekundu na leo Yanga wanaingia nao mkataba logo yao ikiwa na rangi zake.

Hapa nyumbani kampuni zote zilizoingia mkataba na Yanga kwa maana ya kuwa zinatoa fedha, bado Yanga walishindwa kuonyesha heshima na baadaye kulazimika kubadili rangi za logo zao. Mfano mzuri, wadhamini wa ligi Vodacom ambao Yanga wanafaidika nao. Angalia GSM PIA.

Utasikia sisi hatuwezi kufanya kazi na watu wenye rangi nyekundu.

Nimefafanua mara nyingi sana kuwa si kila nyekundu ni Simba au kila njano ni Yanga.

Wadhamini au partners wanapaswa KUHESHIMIWA na vizuri tukaacha "USHAMBA WA RANGI" Hili la @sevillafc na Laliga linaweza kuwa funzo kwa wale ambao kweli hawakuwa wakielewa au wale walikuwa HAWAELEWI KWA MAKUSUDI.
 
Tatizo bodi ya ligi na TFF hawana misimamo, leo hii Azam tv akiwa main sponsor wa ligi kuu watabadili Logo?
 
Tatizo bodi ya ligi na TFF hawana misimamo, leo hii Azam tv akiwa main sponsor wa ligi kuu watabadili Logo?
Watabadili logo tu bodi ya ligi na TFF wamejaa hao hao Simba na Yanga
 
Mimi nilikuwa shabiki wa Yanga, ila hiki kitendo cha kukataa logo ya mdhamini (Vodacom na baadae GSM) kilinifanya nione nashabikia timu ya kipuuzi sana 'isiyojielewa'.
 
Bahati Nzuri kwa Wenzetu ukichezea Logo yao Mahakama na Faini nzito inakuhusu.
 
Mimi nilikuwa shabiki wa Yanga, ila hiki kitendo cha kukataa logo ya mdhamini (Vodacom na baadae GSM) kilinifanya nione nashabikia timu ya kipuuzi sana 'isiyojielewa'.
Mbumbumbu tangu lini akawa shabiki wa Yanga
 
,sisi yanga Wala hatuna tatizo na RoGo ya rangi nyekundu au nyeupe,kutoka nje ya Tz.
 
Story za kipwaguzi hizi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…