Yanga Inapotea, Mwenyekiti anaamua anachokitaka, Aamua kuwakomesha Sekretariati

aka2030

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
2,657
Reaction score
3,679
Hivi karibuni uongozi mpya wa klabu ya Yanga SC chini ya mwenyekiti wake Yusuf Manji uliamua kubadilisha Sekretariati iloyokuwepo baada ya kumaliza muda wake mwezi Novemba 2014, na kutangaza sekretariati mpya chini ya katibu mkuu mpya Dr Jonas Tiboroha, Mkurugenzi wa Fedha Baraka Desdeuth, Mkuu wa Sheria Frank Chacha, Mkuu wa Masoko Omar Kaya na Mkuu wa Idara ya Habari Jerry Muro.

Wanachama wengi walishangazwa na mabadiliko hayo ya ghafla ili hali wafanyakazi waliokuwepo Katibu Mkuu Beno Njovu, Mkurugenzi wa Fedha Denis Oundo, Mkurugenzi wa Masoko George Simba, Afisa Habari Baraka Kizuguto, Mhasibu Rose Msamila na Sekretari Zayana Abdul walikua wakifanya kazi zao vizuri na kwa uweledi mkubwa.

Ila kwa kuwa Yanga ya sasa ni ya mabavu na hakuna mwenye uwezo wa kuhoji juu ya suala lolote kuanzia Kamati ya Utendaji, Wanachama, Baraza la wazee, Mwenyekiti aliyejiongezea muda nje ya katiba ndio amekua na maamuzi yote na kamati yake ya utendaji aliyoiweka haina mamlaka yoyote.

Kutokana na uendeshwaji huo wa mabavu umeipelekea Yanga kuwa na kesi zaidi ya nne FIFA zikisubiria maamuzi, na nyingine katika mahamaka za Tanzania,

Kudhihirisha hilo na kuonyesha Kamati ya Utendaji iliyopo ni hewa, isiyokuwa na maamuzi wal kujitambua kulingana na taaluma zao na nyadhifa mbalimbali walizonazo katika taasisi wanazoziongoza, wamekua ni watu wa ndio katika maamuzi yoyote yanayotolewa yawe mazuri au mbaya kwa maslahi yao na mwenyekiti wao anayewaongoza.

Baadhi yao ni :
Mr Fumbuka - Mkurugenzi wa Core Security
Mohamed Nyegi - Mkurugeni wa Fedha Stanbic Bank
Waziri Barnabas - Mkurugenzi wa Fedha NMB
Seif Ahemd 'Magari' - Mfanyabiashara mkubwa nchini
Isaac Chanji - Afisa Usalma wa Taifa na mwakilishi wa marekani nchini Tanzania kwenye mradi wa Symbion Power
Mosses Katabaro - Kamanda wa CCM Vyuo vikuu nchini na mfanyabiashara mkubwa nchini
Abbas Tarimba - Mkurugenzi wa Bodi ya Bahati Nasibu na mbunge mtarajiwa wa Kinondoni
Clement Sanga - Mhandisi anayejenga miradi mingi ya NHC mjini Dodoma
Sam Mapande - Mwanasheria mkongwe wa CRDB na CCM

Tazama baadhi ya email za maelekezo ya kuwabambikia kesi wafanyakazi hao waliomaliza muda wao kwa lengo la kupoteza na kufunika mabaya yake anayotaka kuyafanya kabla ya kuondoka madarakani kwa mujibu wa vyanzo mbali mbali vya habari kutoka kwa mwanasheria wa klabu ya Yanga Frank Chacha ambaye aliyesaidia kupatikana kwa email hizo kwa lengo la kuwasaidia wana Yanga wainusuru klabu yao isipotelee mikononi mwa mwenyekiti wa Yanga Yusuf Manji.

 
yanga klabu ya wanawake kila mechi wanazimia,yanga ni klabu ya wahuni,yanga ni genge wa wapuuzi,
ukiwa shabiki wa yanga inabidi ukapimwe akili
 

Onyesha tatizo katika hizo email ewe wakala was wezi. Mbona hazina dalili za kubambika kesi? Au umetumwa uje kuwatetea hao watuhumiwa? Aibu yako, huyobkocha msaidizi kapigwa pesa zake, ulitaka mini kifanyike? Acha majungu we we.
 

Attachments

  • image.jpg
    246.3 KB · Views: 182
Onyesha tatizo katika hizo email ewe wakala was wezi. Mbona hazina dalili za kubambika kesi? Au umetumwa uje kuwatetea hao watuhumiwa? Aibu yako, huyobkocha msaidizi kapigwa pesa zake, ulitaka mini kifanyike? Acha majungu we we.

wewe una ushahid wa huyo kocha kupigwq hela zake? Kocha kasema aliazimwa na baada ya kurudishiwa pesa zake anaomba riba ya dolla 500, sasa hapo wizi uko wapi??
 

Sasa mkuu hizi Email zina tatizo gani? na wewe ndiyo nani kati ya wale waliotimuliwa? au wewe ndiyo Beno?.....Yaani nyie mpige hela za Yanga halafu mwenyekiti awachekee!!!? weledi gani mmefanya toka mjiunge na yanga zaidi ya polojo tu! Rudisheni fedha za yanga then ndiyo mje kwenye media kulia lia😡:angry::angry:
 
wewe una ushahid wa huyo kocha kupigwq hela zake? Kocha kasema aliazimwa na baada ya kurudishiwa pesa zake anaomba riba ya dolla 500, sasa hapo wizi uko wapi??

Lete ushahidi. Acha uongo wewe. Kati ya jf na mahakama kipi chombo kinachotoa haki? Kama unadhani huo ndio ukweli so uiache mahakama itende haki? FACT: kwa muda mrefu Yanga na Simba vimekuwa vichaka vya wezi.
 
Nyuma ya pazia huelewi kinacho endelea ndani ya vilabu vyetu

Sasa email inajielezea anatoa maelekezo gani yafanyike, unamkamata mtu kwa wizi ili hali hata auditing haijafanyika?
Amejuaje kama hao watu ni wezi ikiwa wakaguzi hawajafanya ukaguzi?

Pili Yanga ina uwezo wa kuibiwa bilioni 2 ikiwa TBL kwa mwaka anatoa mil 450 na klabu haina biashara nyingine yoyote ya kujipatia kipato:


Kalaghabaho amka wewe
 
Mkuu una hangaika duh! umetupia tena uzi mwingine huku same story!! Mods hebu unganisha hii au toa hapa!
 

Kumbe akili yako finyu sana. Acha kujaza server bure.
 
yanga klabu ya wanawake kila mechi wanazimia,yanga ni klabu ya wahuni,yanga ni genge wa wapuuzi,
ukiwa shabiki wa yanga inabidi ukapimwe akili

Utakuwa kwenye siku zako wew...kama haikuhusu kaa kimya
 
Mwenyekiti anaweendesha kama hivi ehh
 

Attachments

  • yanga.jpg
    30.1 KB · Views: 212
wewe una ushahid wa huyo kocha kupigwq hela zake? Kocha kasema aliazimwa na baada ya kurudishiwa pesa zake anaomba riba ya dolla 500, sasa hapo wizi uko wapi??

Beno na Rose mmekuja kuomba poo JF?subirini Manji keshawashikia chini.kama ulikuwa ni mkopo mbona Leiva aligoma kuondoka mpaka apewe pesa zake? na Je ni taratibu za kazi kwa katibu au mhasibu ku reallocate funds without proper cause? tumeambiwa kuwa kuna wafanyakazi hawana mkataba na Yanga lakini wanakula mshahara, kuna watu walishamaliza muda wao wa utumishi lakini bado walikuwa wanalipwa mishahara.Kama kina Beno sio wezi tusubir audit report mbona wana gwaya gwaya.?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…