Yanga kimasihara mnapoteza ubingwa

Shida iliyopo timu za taasisi hazita miamala ya utopolo ila mechi ijayo watashinda
 
Mkuu umeandika kwa uchungu sana...

Ila unavyojisikia leo, ndivyo walivyojisikia wengine kipindi kingine. Kuimba kupokezana. Pole sana.
 
Manara kazi yake ya andakava anaifanya vizuri
 
Kilichofanyia ni kumpambania Maleye dhidi ya mpole. Nimeshangaa sana.
Timu anajari rekodi za mtu binafsi kuliko timu yenyewe itatuchukua miaka mingi kujielewa
 
Mtasema mengi ila ukweli ni kwamba,;
1. Utopolo wameathiriwa na siasa za mitandaoni na wachambuzi waliopewa bahasha ya khaki na gsm wakiwaaminisha watu kuwa hakuna kama mayele.

2. Timu nyingi zinahofu ya kushuka daraja na kwa hiyo hawapokei tena bahasha.


Kwa hiyo sasa ndio wakati wa kuiona utopolo halisi
 
Timu anajari rekodi za mtu binafsi kuliko timu yenyewe itatuchukua miaka mingi kujielewa
Feisal alikuwa ana nafasi ya kufunga mwenyewe eti anampa pasi Mayele ili afunge yeye. Penati Djuma Shaban kauchukua mpira nikajua anaenda kupiga yeye, nashangaa mpira upo kwa Mayele kile kiliniudhi japokuwa sikujua kama atashinda au atakosa.

Wachezaji wana option nyingi ya kutoa mipira kwa wengine lakini wao kila mpira kwa Mayele. Kuna tatizo kubwa la mentality kwa wachezaji wa Yanga.
 
Mpiga penalty wa timu alikuwa bize uwanjani akifanya ulozi

 
Mimi ni Simba damu damu nikiri tu wazi Yanga atakua bingwa huu msimu no matter what.
Ila kinachonipa furaha ni kwamba yanga atakua bingwa kwa utofaut wa points chache tofaut na wao walivyokuwa wanataka ,pia watachelewa kidogo kutangazwa kuwa mabingwa.

Ishu ya pili ambayo naweza sema inawatafuna yanga ni ujinga wa kutaka afunge mayele tu ,jaman yule ni mchezaji na timu ni nembo ,wangapi walipita yanga na wakaiacha?

Yaan mtu amekuja yanga Ana follow buku tano tu now Ana followers kibao huko ig na kwa ujinga wetu sisi watz tunaabudu Sana wachezaji wa nje kuliko hata nembo za vilabu vyetu.

Leo hii furaha ya Wana yanga imebebwa na mayele kias kwamba kila mchezaji anampambania mayele ili wapate kutrend mitandaoni ,huo ni ufala kabisa watani zangu mbadilike kabisa na wachezaji waambiwe kuwa kila mchezaji anapaswa kufunga .
 
Mpigaji penati kila siku anajulikana n shaban djuma Sasa mayele aliendaje pale kupiga penati?
Mayele aling'ang'ania, maana Shaban Djuma hapa chini alikuwa anaenda kuuchukua mpira apige, Mayele akakataa ili awe mfungaji bora

 
akipata majeruhi ya mda mrefu sijui watafanyaje
 
Kwenye mpira kuna mambo mengi, usikate tamaa nafikiri matokeo ya Mtani ndiyo yatuchanganya, ila nafasi ya ubigwa ni kubwa sanaa, ujinga walioufanya wachezaji kuwaona preson ni underdog kwakuwa tulifunga kwao game ya kwanza
 
Nazani hii yakumpambania Mayele ni maelekezo kabisa toka kwa walimu..
kuna mechi moja nazan ni ile ya simba nilimsikia Kaze akisema wachezaji walikuwa hawampatii Mayele pas nzur zakufunga
 
Kwahiyo Sasa baada ya yanga kutoa draw mechi tatu MSIMAMO WA LIGI UPOJE?.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…