Yanga kumtupa nje Manji na kugeuka kampuni

kedrick

JF-Expert Member
Joined
Apr 25, 2015
Posts
5,080
Reaction score
4,914
Habari ya town ni kuwa kesho katika mkutano wa Yanga wanachama wana mpango wa kufanya mabadiliko ya kuwa kampuni na kumnyanganya timu mfadhili wao Manji na kumpa timu tajiri mwingine ambaye yupo tayari kununua hisa asilimia 55 za Yanga kwa Shs bilioni 50 uku akihaidi kuwajengea uwanja wa mpira wenye hadhi wa kimataifa, hostel za wachezaji na jengo jipya la klabu iyo.
 
Wahindi na Soccer... Ngoja tuone mwisho wake....
 


Mkutano ni wa ghafla na umeitishwa na mwenyekiti ambae ni manji wala haujaitishwa na wanachama. Ingekua inakula kwa Manji mkutano ungeitishwa kwa shinikizo la wanachama.
 
Inogile
 
Mkutano ni wa ghafla na umeitishwa na mwenyekiti ambae ni manji wala haujaitishwa na wanachama. Ingekua inakula kwa Manji mkutano ungeitishwa kwa shinikizo la wanachama.
Embu nitajie agenda za mkutano km unazijua [emoji6]
 
Embu nitajie agenda za mkutano km unazijua [emoji6]


Mwenyekiti ndie aliyeitisha kikao na hukukua na mgogoro wowote bado ajenda ni siri ya mwenyekiti hata wanachaa hawajui.
 
.....presha tu zinawapanda majirani baada ya kusikia "MO"
tulieni,mjiandae kuucheza mziki!
 
Embu nitajie agenda za mkutano km unazijua [emoji6]
AGENDA
1) BARUA YA MAJIBU KUHUSU UWANJA
2) MAANDALIZI LIGI KUU
3) KLABU KUWA KAMPUNI
4) UDHAMINI QUALITY GROUP
5) MAPUNGUFU YA UONGOZI KAMATI YA UTENDAJI NA UONGOZI WA JUU

HIZO NDIYO AGENDA ZA JMOS, YANGA MBELE NYUMA MWIKO TUHUDHURIE DAIMOND JUBILEE WANACHAMA YANGA..

Ukitoka kujua zaidi nenda makao makuu leo kuna Press conference
 
Usitupe mbachao kwa msala upitao
 
Iyo namba 3 na 4 ndo inagojewa lazima mshikane mashati
 
Mkutano ni wa ghafla na umeitishwa na mwenyekiti ambae ni manji wala haujaitishwa na wanachama. Ingekua inakula kwa Manji mkutano ungeitishwa kwa shinikizo la wanachama.
That is common sense mkuu. Huyo jamaa atakuwa mzushi tu
 
Huyo jamaa apewe kwa billion 30 tu. Hizo 20 akanunue Simba iwe academy ya Yanga. Teh teh teh
 
MO alishindwa Singida United,African Lyon simba NATO atachemsha.Mashamba ya katani,chai kayashindwa

.....wewe kweli bongolala!, yaani unailinganisha Simba na Singida Utd?!
 
Hiyo no 5 nahisi ndo itatawala mkutano ikiwa ni pamoja na kuwashitaki baadhi ya wajumbe wa kamati tendaji kwa wanachama ili wawafukuze.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…