Kaka nitatia team pale Mjengoni baadaye kupata hali halisi ya leo(siku 1 baada ya kuvuliwa nguo jana) lakini kwa jinsi ninavyofahamu mimi tatizo pale ni uongozi,viongozi wameshindwa kuendesha team kiufanisi,wachezaji na makocha hawalipwi mishahara kwa wakati,hakuna umoja kabisa makundi mengi yamezaliwa,viongozi waliokuwa na msaada mkubwa kuliko hata huyo Mwenyekiti wamejiengua kama kumsusia team hivi na hata kama umeangalia ile mechi utaona wachezaji wa Yanga walikuwa wanacheza ilimradi wameugusa mpira hakukuwa na morali ile tuliyoizoea wanayokuwaga nayo siku wanayocheza na Simba,na ni kama vile kuna wachezaji waliokuwa wameandaliwa(pengine labda na kundi fulani) kutengeneza matokeo ya namna ile na ndo maana ilifika kipindi hata kipa Said Mohamed alitaka kugomea penalt moja.
Sasa kwa maoni yangu,kinachotakiwa kufanyika ni:-
1.Uongozi kuondoka,wa'resign tuchague watu wenye uwezo wa kuiendesha Yanga kiufanisi.
2.Kupunguza wachezaji wote wasio na manufaa kwa team ambao wanaweza kufikia hata 20,na kusajili wengine watakaoweza kuiletea Yanga matokeo chanya.
3.Kubadili benchi zima la ufundi,Papic aachwe aende zake na Minziro hana jipya amesha'prove failure mara zote alizoachiwa team,watafute kocha mpya kutoka nje.
4.Kurudisha umoja kati ya Viongozi na Wapenzi wa Yanga wenye uwezo wa hata kuisaidia team kwa fedha zao binafsi pale inapolazimika.
Mwanachama wa Yanga.