Yanga kuvaa nembo ya mdhamini sio haramu

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Nembo ya Vodacom ina wekundu na weusi kitu kinachowapa kigugumizi wenzangu wa Yanga kuweza kuivaa kwenye jezi zao kama ilivyo eti kuepuka lile doa nyekundu kwenye nembo. Miaka iliyopita walilazimisha nembo hiyo kubadilishwa rangi na kuwa nyeusi. Hii nadhani sio Sawa Kwa wenzangu wa Yanga kwakuwa rangi nyekundu sio ya Simba na ilikuwepo hata kabla ya Simba kuanzishishwa. Damu zetu ni nyekundu, sare za wanajeshi zina wekundu, nishani zina wekundu, mapapai yako mekundu, madaladala yako yenye rangi nyekundu na nyama ni nyekundu. Kuvaa nembo Tu hakutoshi kuinajisi jezi yote kuwa haifai kwasababu kinembo cha Vodacom kina wekundu.

Hela ya mdhamini tunataka lakini nembo yake hatuitaki. Tuache ukorofi na ushamba kwenye hela za watu.
 
Sijui ni kweli nasikia kuanzia hakimiliki ya nembo ya yanga hadi hatimiliki ya kuonyesha matangazo bado anamiliki manji sasa sijui mtu mzima salaah kashainunua mbaya zaidi GSM rangi nyekundu kwe lebo yao za kumwaga...ngoja tusubiri
 
Haramu itakuwa Simba kuvaa kijani. Si ndivyo?
 
acha kufananisha unazi wa timu na vitu vya kijinga wewe
Mtu anatoa pesa yake halafu tunatanguliza nyodo ya kumtaka mtu abadilishe rangi ya nembo yake, khaaaa, tangu lini rangi ya nembo ikasababisha rangi ya jezi kubadilika? Tuache hizi tuandae timu vizuri na tuwalipe wachezaji na kocha vizuri timu itapata matokeo Tu hata kama nembo ikiwa nyekundu au blue
 
Reactions: BAK
hvi
kuna timu ulaya yenye case kama hii?
 
Kiuhalisia nembo ya Vodacom ni nyekundu na nyeupe, tunapomlazimisha nembo yake iwe nyeusi ni kumlazimisha mfadhili atende kosa huko brella na kwingineko bila sababu ya msingi. Hebu vitu vidogovidogo tuvivumilie Tu.
 
hvi

kuna timu ulaya yenye case kama hii?
Ulaya hawana upumbavu wa kuweka nembo ya mdhamini wa ligi kwenye jezi za timu. Barclays Bank haikuwa na na nembo yake kwenye jezi za timu.
Kila timu ina mdhamini wake Wa jezi. Akina Adidas, Puma etc.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…