benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,533
- 3,187
Mapema leo, NBC Bank na TFF zimeingia ubia wa udhamini wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara, NBC wakiweka mezani bilioni 7.5 kwa kipindi cha miaka 3.
Moja kati ya faida anazotarajiwa kupata NBC Bank kama mdhamini ni uwepo wa nembo/chapa yake (Logo Placement), katika jezi za timu shiriki katika Ligi Kuu.
Nembo rasmi ya NBC ina Twiga pamoja na Mlima Kilimanjaro, lakini kimbembe ni kwamba Twiga aliyepo kwenye nembo hiyo ana rangi nyekundu, rangi ambayo pia ipo kwenye logo ya Vodacom.
Rangi hii ndio ambayo mabingwa wa kihistoria Dar Young Africa waligoma isiwepo katika jezi zao. Swali hapa ni je, nini kitatokea kwa rangi ya mdhamini katika jezi watakazovaa wananchi.
MUDA UTATUPA MAJIBU, TUSUBIRI TUONE.
Moja kati ya faida anazotarajiwa kupata NBC Bank kama mdhamini ni uwepo wa nembo/chapa yake (Logo Placement), katika jezi za timu shiriki katika Ligi Kuu.
Nembo rasmi ya NBC ina Twiga pamoja na Mlima Kilimanjaro, lakini kimbembe ni kwamba Twiga aliyepo kwenye nembo hiyo ana rangi nyekundu, rangi ambayo pia ipo kwenye logo ya Vodacom.
Rangi hii ndio ambayo mabingwa wa kihistoria Dar Young Africa waligoma isiwepo katika jezi zao. Swali hapa ni je, nini kitatokea kwa rangi ya mdhamini katika jezi watakazovaa wananchi.
MUDA UTATUPA MAJIBU, TUSUBIRI TUONE.