Yanga na Simba zinapokuwa Bungeni

Hata ulaya wanavaa suti,acheni kuwa wachafu wachafu
 
Kwanza hii tabia ya kwenda bungeni sijui nini ni hapa bongo sijui Manchester city kama watafanya hivo
Acha inferiority complex......kwahio kitu tunachofanya lazima ulaya wafanye??

Unajua kama mshindi wa NBA huwa anaenda white house.? Hio mbona husemi?
 
POZI LA HAJI MANARA BUNGENI DODOMA, ANALIJUA MWENYEWE...






Mabingwa wa soka Tanzania, Simba wamealikwa bungeni mjini Dodoma kwa mwaliko wa Spika wa bunge hilo, Job Ndugai.

Simba walihudhuria bungeni na kila mmoja alikuwa na pozi lake, kama unavyojua, wachezaji hawajazoea kukaa muda mwingi, hayo ni mambo ya kiofisi, wao wanapambana uwanjani.

Pamoja na yote, pozi la kuvutia zaidi lilikuwa ni la Msemaji wao, Haji Manara ambaye aina yake ya ukaaji, ilionekana kuwavutia wengi.

Manara alionekana kukaa kama mtu aliyekuwa anataka kupaa hivi, ukaaji wa maringo na kujiamini, hali iliyokuwa ikitafsiri furaha yake ya ubingwa.

Kila Simba ilipofeli kupata ubingwa, Manara amekuwa ndiye mtu anayeandamwa zaidi na watani wake wa jadi, Yanga kwa kuwa amekuwa akiwachemsha mfululizo.

Lakini tokea Simba imechukua ubingwa, inaonekana wazi Manara ana ahueni kubwa na hata muondoko wake, kiasi umeongezeka mikogo.

Amekuwa akisisitiza kwamba atazungumza sana na Yanga wajiandaa kwa kuwa Simba imechukua ubingwa unaostahili, maana ni ubingwa wa halali maana kabla ya mechi tatu, tayari walibeba ubingwa na si suala la kutofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa.
 
Yanga wameishazoea kwenda Bungeni. Hamna kitu kipya. Jamaa zetu baada ya miaka mitano, ndiyo wamepata nafasi. Ni sawa na mtoto anaevaa nguo mpya siku ya Eid au Christmas tu. Lazima awe mshamba na nguo hiyo.
 
Mbona sijawahi sikia Chelsea au Arsenal wakienda bungeni UK
 
Mikia inabidi kwanza nyinyi wenyewe mjikubali kua ni MABINGWA wa VPL kwa msimu huu maana naona mmewehuka na hamuamini kama ni mabingwa hizi comparison ni mfano wa mengi yanayoendelea kwenye mitandao.
Nimeamini jamaa wali-miss haswaa kuwa mabingwa [emoji23][emoji23] maana wanatamani hata siku ya kupewa kombe iwe sikukuu ya kitaifa.
 
Ningeona tofauti kama Simba wangevaa Suit
Bila hivyo naona kitu kimoja hapo juu tofauti ni rangi tu
 

Sasa mtoto ameanza la kwanza hadi akamaliza la saba ubingwa hamna unadhani hiyo arosto mchezo?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ni upumbavu tu na kuingiza siasa kwenye Moira ndo maana Moira wetu unashuka kila siku!....wachezaji wana tabia za kimasikini kwenda kuombaomba hela kwa wabunge Kyle ndo dhumuni LA kwenda!....shit!
.
 


Compare and Contrast
Simba huu ulimbukeni,ushamba na umbumbumbu mtaacha lini?. Kwanini msisubiri mkabidhiwe kombe mwende bungeni angalau mpige nalo picha kuliko kwenda mikono mitupu as if wajinga fulani hivi!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…