Yanga na teams zote za ligi kataeni huu upuuzi

kishumbaz

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2015
Posts
1,183
Reaction score
1,619
Ushabiki tuweke kando, ligi yetu ya Tanzania bara ipo corrupted, kuanzia daraja la kwanza ndiyo madudu kabisa, ligi kuu bingwa anaandaliwa kabla ligi kuchezwa

Tatizo lipo TFF, nachelea kusema bodi ya ligi au chama cha marefa....sababu TFF wanajua kabisa madudu ya hizi idara na wana mandate ya kuzivunja wapo kimya.

Ushauri wangu kama hakutatokea mabadiliko kwenye hizo sehemu hapo juu...tutegemee simba kuchukua ubingwa misimu yote mpaka mabadiliko ya uongozi wa TFF, chama cha waamuzi na bodi ya ligi vipo corrupted.
 
kwa ufatiliaji wako wa soka umewahi sikia timu ina viporo 12

ama timu kucheza kila baada ya siku 2

ama backpass kuwa offside

ama mpira kuendelea ikiwa golikipa kaumia
Unazijua sheria za mpira vizuri? Fuatilia kuhusiana na kipa kuumia halafu yupo nje ya mstari nini kinatakiwa kufanyika?
 
Ndugu leo hii ndio unajua kuwa tff ni wapiga dili, au kwakuwa zahera kakuaminisha hivo!? Moja ushaonekana upo upande gani! Malalamiko ya kocha wa yanga juu ya kupendelea timu fulani emu kaa chini na ujaribu kufikiria zile points zake utagundua kitu ndugu, !! FA kakosa , mapinduzi kakosa, sportpesa kakosa, kama kweli tuhuma zake ni kweli je kwanini hayo mengne hajachukua? Tatizo la waamuzi kwene ligi yetu lipo toka muda na bado TFF huwa kimya au sometime hufanya maamuzi kwa kukurupuka!! Kama umeanza fatilia ligi yetu toka muda ungeshagundua kitu na nahisi ungeeleweka zaidi
 
Unazijua sheria za mpira vizuri? Fuatilia kuhusiana na kipa kuumia halafu yupo nje ya mstari nini kinatakiwa kufanyika?
Hawajui ndugu yangu , hao wamerishwa matango pori na kocha wao anaejua kila kitu kumbe hamna kitu
 
Mkuu, hebu kuwa fair kidogo basi. Kwa maandalizi yalivyokuwa (kuanzia usajili hadi kambi ya pre-season), hivi kweli Simba haikutarajiwa kubeba ubingwa? Ni timu gani unadhani ilitarajiwa ukiondoa Simba?Yanga hii ambayo kocha wake alikiri kabisa kwamba wakikutana na Simba, njia rahisi ya kuzuia magoli ni kupaki bus? Wakati mwingine muwe mnaangalia mizani basi, daah!
 
sijaongelea yanga pekee...nmeongelea yanga na team zote za ligi kuu..soma uelewe
 
kwa ufatiliaji wako wa soka umewahi sikia timu ina viporo 12

ama timu kucheza kila baada ya siku 2

ama backpass kuwa offside

ama mpira kuendelea ikiwa golikipa kaumia
Hata ingetokea nyie mngeshiriki ligi ya mabingwa mpk hatua waliofika wenzenu basi nanyi pia mngekuwa na viporo hvyo. Kwahyo tulia dawa iingie vizuri
 
kufungwa siyo tatizo, tatizo je ulifungwa kihalali....kuna figisu za kupangiwa matches za mbali mfululizo..mfano Tanga to singida then Tanga tena ukitoka hapo Lindi...makusudi tu..magoli halali kukataliwa...kunyimwa penalt za wazi nk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…