demigod
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 8,292
- 15,250
Ni nani hasa anayeruhusu uhujumu uchumu wa Klabu ya Yanga SC kwenye suala zima la jezi.?
Ni kiongozi yupi wa Yanga SC asiyejua kuwa suala la jezi lina maslahi mapana kwa klabu.?
Nimekuwa nikifuatilia hizi jezi Mpya za Yanga ambazo zinasemekama zinaenda kutumia msimu ujao wa 2017/18. Hizi jezi zinauzwa kama njugu, cha ajabu zaidi ni kwamba Klabu haipati mgawo wowote ule kutoka na na mauzo ya Jezi hizi.
Ni tofauti sana wanavyofanya klabu kubwa nyinginezo ambapo percentage ya mauzo ya jezi ya klabu husika yanarudi klabuni. Hivyo kuifanya klabu kuwa na chanzo cha ziada cha mapato.
Ebu Fikiria: Jezi moja tu inauzwa kwa Tsh 20,000/= ambapo hakuna hata senti 5 inayoingia klabuni. Ni biashara gani hii wanayoifanya YANGA SC?
Bila shaka kuna kiongozi mule ndani anahusika moja kwa moja na dili hili ambapo kwa story za chini ya kapeti zinasema yeye pekee anavuta ka'mkwanja kwa kuidhinisha utengenezaji wa hizi jezi na huyo mzalishaji.
Nataka viongozi wangu watambue kuwa Yanga ni Brand kubwa sana, iweje suala la jezi linamnufaisha mtu binafsi na sio klabu. Na hapo hapo tunalazimika wanachama kuchangia klabu inapoonekana hakuna pesa za kutosha kuendesha klabu.
Ni kiongozi yupi wa Yanga SC asiyejua kuwa suala la jezi lina maslahi mapana kwa klabu.?
Nimekuwa nikifuatilia hizi jezi Mpya za Yanga ambazo zinasemekama zinaenda kutumia msimu ujao wa 2017/18. Hizi jezi zinauzwa kama njugu, cha ajabu zaidi ni kwamba Klabu haipati mgawo wowote ule kutoka na na mauzo ya Jezi hizi.
Ni tofauti sana wanavyofanya klabu kubwa nyinginezo ambapo percentage ya mauzo ya jezi ya klabu husika yanarudi klabuni. Hivyo kuifanya klabu kuwa na chanzo cha ziada cha mapato.
Ebu Fikiria: Jezi moja tu inauzwa kwa Tsh 20,000/= ambapo hakuna hata senti 5 inayoingia klabuni. Ni biashara gani hii wanayoifanya YANGA SC?
Bila shaka kuna kiongozi mule ndani anahusika moja kwa moja na dili hili ambapo kwa story za chini ya kapeti zinasema yeye pekee anavuta ka'mkwanja kwa kuidhinisha utengenezaji wa hizi jezi na huyo mzalishaji.
Nataka viongozi wangu watambue kuwa Yanga ni Brand kubwa sana, iweje suala la jezi linamnufaisha mtu binafsi na sio klabu. Na hapo hapo tunalazimika wanachama kuchangia klabu inapoonekana hakuna pesa za kutosha kuendesha klabu.