BAO pekee la dakika ya 17 ya mchezo wa leo mjini Curepipe, Mauritius lililofungwa na Mzimbabwe Donald Ngoma dhidi ya limeisafishia tu Yanga njia dhidi ya Cercle de Joachim kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, lakini bado halijawapa uhakika wa kufanya vizuri kwenye mashindano ya mwaka huu.
Matokeo ya mchezo huo wa kwanza, ambao dhahiri ulikuwa wa ushindani mkubwa kutokana na soka la kasi linalochezwa na mabingwa hao wa Mauritius, hayatoi nuru ya kutosha kwa vijana wa Jangwani ambao wamekuwa na rekodi ya kuzionea timu kutoka Visiwa vya Bahari ya Hindi hususan Mauritius, Comoro na Shelisheli.
Faraja pekee inayoweza kuelezwa na wadau wa soka ni kwamba, timu hiyo ilikuwa inacheza ugenini, hivyo inayo nafasi ya kutosha kujirekebisha na kufanya vizuri kwenye mchezo wa marudiano utakaofanyika Februari 27, 2016 jijini Dar es Salaam.
Hata hivyo, kwa mwenendo ilionao timu hiyo, hata kama itavuka hatua hiyo ya awali, inaweza kurudia raundi ya pili, tena Kigali, mbele ya APR.
SOMA ZAIDI...