Yanga wakabidhiwa jezi zao na mdhamini wao mkuu SportPesa leo!

Wonderful

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2015
Posts
7,347
Reaction score
5,986

Hatimaye Yanga wamekabishiwa jezi zao za msimu ujao na wadhamini wao SportPesa.

Yanga ilicharuka baada ya jezi zao kukabidhiwa na kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom ambao ni wadhamini wa Ligi Kuu Bara.

Lakini leo, Yanga wamekabidhiwa jezi hizo na Abbas Tarimba, mmoja wa Wakurugenzi wa Sportpesa.

Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu ya Yanga, Salum Mkemi ndiye aliyepokea jei hizo.
 
Yanga wajue hawawezi kutumia hizi jezi bila ya kubandika logo ya mdhamini mkuu. By the way mbali na hizi kutokuwa na logo zina tofauti gani na zile walizogawa Vodacom juzi?
 
Haji Manara keshazishika, haijalishi! Mikono yake ilitokea kamati ya ufundi kabla ya kufika pale.
 
Mbona hiyo logo ya sportpesa imeshuka sana haipo center of the jersey.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Manara kazirudisha ?
Kwanini hawakuchukulia kwake ? Kwani kuna tatizo gani ??
Mdau wa michezo, mtani kakuta jezi ukumbini watani hawapo kawachukulia kiungwana kabisa sasa hawazitaki kwanini?
Kwani Manara kafanya kosa kufanya uungwana kiasi kikubwa vile. Kwanini hawakujali uungwana wake wakapokea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…