Yanga wako serious kumtaka Khama Billiat

Unai Emery

Member
Joined
Nov 19, 2019
Posts
79
Reaction score
62
Yanga wako serious kumtaka Khama Billiat...Ni mchezaji mzuri sana!

Hakuna shaka juu ya uwezo wake, kama atafikia asilimia 50 tu ya uwezo wake ninaoujua atasumbua na kuimbwa sana!

Changamoto ya nyota huyo wa Kimataifa wa Zimbabwe ni majeraha ya muda mrefu...

Tangu akiwa Mamelodi Sundowns alikua na changamoto kadhaa kama Misuli,Nyonga,goti na msimu 2016/2017 aliwahi kukaa siku 37 akiuguza majeraha yasiyojulikana...Sawa na siku 97 alizokaa akiuguza majeraha yasiyojulikana akiwa na Kaizer Chiefs.

Akiwa Kaizer Chiefs,Khama ameendelea kukumbwa na majeraha ya Goti (Knee Injury) Achilles tendon problems,Hamstring Injury,Fractured Leg na sasa tatizo la kinena (Groin Injury) limemuweka nje kwa siku 145.

✍️ Sospeter Ilagila
 
Naona mmeona Simba wanafaidi sana kuwa na Sawadogo mkaona na nyie mtafute wenu
 
Mimi naona wangeachana naye tu. Kwanza umri wake wenyewe umeshamtupa mkono. Miaka 32 kwa timu inayo jijenga kama Yanga, ni kupoteza tu hela.

Yanga inatakiwa kusajili wachezaji vijana wenye vipaji vikubwa, kwa ajili ya kuja kuchukua nafasi za akina Aucho, Mayele, nk. Na siyo hao wazee na majeruhi kama Khama Billiat.
 
Ni kweli kabisa mkuu, sasa hivi kumekuwa na utapeli mkubwa sana kwenye biashara ya wachezaji, naona ni vema tukabadilisha strategies hata haikuwa sawa sana Rais Harsi Kumuingizia juu ya mchezaji wanafikiria kumsajili sasa, kwani inaleta picha mbaya kidogo kwa wachezaji waliopo hasa kwenye kipindi hiki timu ipo kwenye michezo muhimu sana.
 
Ni sahihi ila kwa uchumi wetu bado kabisa kufikia hizo level unazozisema ,sisi bado hatujafika level za kuvunja mikataba ya wachezaji wazuri walio katika timu shindani...

Jiulize kuwa unaweza kwenda pale mamelod na ukamuapproach Peter Shalulile au Themba Zwane na ukafanikisha deal????

Je,tunaweza kwenda pale Raja CA tukamshawishi Hamza Khaba ajiunge nasi??

Vipi unaweza fika Ahly kumshawishi Kahraba, jibu ni NO, WE CAN'T DO IT.

sisi hawa free agent,wazee wa pension na fairule wa ligi kubwa ndio wa kwetu kwasasa...huko tutafika ila bado....

Lazma tuboreshe haya kwanza

1.MIUNDOMBINU
2.UBORA WA LIGI
3.UCHUMI WETU
 
WANANCHIIIIIIIIIIOOOOOOOOO. LEO NDIO ILE SIKU AMBAYO WANAYANGA WOTE TUNA BANG NAYO .
YAANI MAKOLO LEO NDIO RASMI WANAGEUZA VYOO MAHALA PAO PA KULILIA.
TUNAENDA KUTINGA FAINALI RASMI KWENYE ARDHI YA UGENINI.
MARK MY WORDS
 
Tukatafute wachezaji wasio na matatizo ya kiafya. Hawa wenye mishono hadi kwenye moyo, waache waende Simba
 
Kwa viongozi wa Yanga walivyo makini sidhani kama wako siriazi kumsajili Khama Biliat. Ni kweli ni mmojawapo wa wachezaji wazuri sana anapokuwa fit. Ila jamaa ni majeruhi muda mwingi anautumia kwenye matibabu kuliko kuwa uwanjani.. Aliye karibu na injinia amsanue kama hajui kuwa jamaa na majeraha ni pipa na mfuniko.
 
Umri, majeraha, wanamtaka wa kazi gani sasa? Hebu waache uduanzi.
 
Tatizo la vilabu vya Tanzania ni liquidity problem, havina pesa na ndio maana vinategea kumsajili bure mchezaji aliyetemwa baada ya umri kumtupa mkono.

Na pale wanapotaka kumsajili wanaweka watu wao kwenye mitandao pamoja na kuvihonga vyombo vya habari ili kumfagilia huyo mchezaji alivyo 🔥 wa kuotea mbali ili mradi tu lengo lao la kumsajili litimie.

Baada ya hapo wakisha msajili ndio huyo mchezaji anapokuja kuumbuka pale anaposhindwa kukidhi matarajio ya kusajiliwa kwake na tumeona kwa wachezaji kadhaa hasa wa kigeni baada ya kushindwa kuwepo kwenye starting eleven au hata kwenye substitute bench.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…