bryan2
JF-Expert Member
- Jun 8, 2016
- 3,323
- 4,679
Mpaka Kipenga cha Mwisho Yanga 1 Simba 1.
Nimefuatilia mpira kwa ukaribu Yanga wamejenga mashambulizi ya hatari sana kuliko Simba na wamepiga mashuti mengi yaliyolenga goli kuliko Simba wakiwa wamepiga mashuti 9 yaliyolenga goli.
Yanga waliingia kwenye mchezo huu wakipewa nafasi ndogo kabisa ya ushindi huku wapinzani wao wakipewa nafasi kubwa na hata vyombo vingi vya habari na wachambuzi mbalimbali wa kabumbu waliwapa Simba Nafasi kubwa ya Ushindi.Hii ni kutokana na usajili wao wa bilioni kadhaa waliofanya wakichagizwa na wachezaji kama Niyonzima,Nyoni,Okwi wao wakimwita kiboko ya Yanga,Boko na Manula.
Sifa kubwa kwa Simba apewe Kipa wao Aishi Manula kwa kuokoa michomo ya hatari langoni mwake huku kwa Yanga wapewe wachezaji wote kwa kucheza kitimu zaidi,Na pia wachezaji muhimu wa Yanga kama Ngoma,Tambwe,Kamusoko wamekosa mchezo wa leo kwa sababu za majeruhi.
Pia Simba waliuchukulia mchezo huu kwa umakin zaidi wakisema Yanga anakula bakora 7 leo na kuweka Kambi Zanzibar huku Yanga wakibaki Bara na Simba kufikia hoteli ya Serena huku Yanga wakifika hoteli za kawaida tu.
Bravo Lwandamina na Nsajigwa.
Nimefuatilia mpira kwa ukaribu Yanga wamejenga mashambulizi ya hatari sana kuliko Simba na wamepiga mashuti mengi yaliyolenga goli kuliko Simba wakiwa wamepiga mashuti 9 yaliyolenga goli.
Yanga waliingia kwenye mchezo huu wakipewa nafasi ndogo kabisa ya ushindi huku wapinzani wao wakipewa nafasi kubwa na hata vyombo vingi vya habari na wachambuzi mbalimbali wa kabumbu waliwapa Simba Nafasi kubwa ya Ushindi.Hii ni kutokana na usajili wao wa bilioni kadhaa waliofanya wakichagizwa na wachezaji kama Niyonzima,Nyoni,Okwi wao wakimwita kiboko ya Yanga,Boko na Manula.
Sifa kubwa kwa Simba apewe Kipa wao Aishi Manula kwa kuokoa michomo ya hatari langoni mwake huku kwa Yanga wapewe wachezaji wote kwa kucheza kitimu zaidi,Na pia wachezaji muhimu wa Yanga kama Ngoma,Tambwe,Kamusoko wamekosa mchezo wa leo kwa sababu za majeruhi.
Pia Simba waliuchukulia mchezo huu kwa umakin zaidi wakisema Yanga anakula bakora 7 leo na kuweka Kambi Zanzibar huku Yanga wakibaki Bara na Simba kufikia hoteli ya Serena huku Yanga wakifika hoteli za kawaida tu.
Bravo Lwandamina na Nsajigwa.