Yanga wamejipanga sana. Wanawezaje kumiliki vipindi vyote vya michezo nchini na kuwalazimisha kusema agenda zao?

kibaravumba

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
6,634
Reaction score
7,015
Leo nimesikia Senzo amekamatwa kwa sakata la tuhuma za kumaswa kwa mawasiliano yake akishawishi mmoja ya watu wa Simba ili Simba ihujumiwe kwenye mechi zake na kama tulivyoona hasa mechi ya prisons.

Hata hivyo suala hili zaidi ya kuliona kwenye akaunti za insta ambazo nyingi zimejaa umbea na si za kuaminika,sijasikia vyombo vya habari vikiliongelea. Badala yake, ninasikia umbea wa mara Chama amesajiliwa Yanga, mara Onyango ana corona! Na wamefanikiwa sana kuvuruga mijadala ya matukio halisi yanayotokea.

Kwa jinsi hii naona kweli yanga wamewekeza sana nje ya uwanja na bila shaka hadi nje ya nchi ili kuleta propaganda za kuwaangusha watani zao Simba.

Nakubali kauli ya Eng. Hersi kuwa yanga isipochukua ubingwa, walaumiwe wao.Hizi nguvu za kuteka vyombo vyote vya habari, imenitisha.
 
Hata siku ya mechi simba na yanga watangazaji wa radio one walikuwa wanaonyesha ushabiki WA wazi wazi... Yaan mashambulizi Goli LA yanga hakuna bashasha na hata simba wakigusa Mpira mtangazaji anakuwa slow sana. Nadhani walijipanga Sana yanga kupenyeza rupia kwa vyombo vya Habari
 
Viongozi wanatuhujumu, wachezi wanatuhujumu, vyombo vya habari vinatuhujumu..

Senzo Ametuhujumu tumemfunga.. ila ameachiliwa huru kwa sababu hatuna ushahidi..

Haji manara ametuhujumu Ametukana waandishi wa habari ona sasa hawatupi kiki..! yeye anatangaza magodoro ya GSM..! dah tumebaki na diamond tu
 
...Badala yake,ninasikia umbea wa mara Chama amesajiliwa Yanga,mara Onyango ana corona!Na wamefanikiwa sana kuvuruga mijadala ya matukio halisi yanayotokea.
Mkuu inawezekana wewe umenipa jibu la swali nililokuwa ninajiuliza. Leo nilikuwa najiuliza, kama Yanga wamemsajili Chama, basi atacheza kuanzia msimu ujao, yaani Julai 2021, na kama atacheza mwezi Julai mwakani, kwa nini Yanga wanairipoti sana habari hii leo, amabapo ni miezi zaidi ya nane kufikia siku ya Chama kuweza kusaini na kucheza Yanga? Kumbe inawezekana kweli wanaiweka habari hii kuteka mjadala mwingine
 
MIkIa fc.
 
Nimeona hata mwanaspoti wameandika habari za Senzo kuachiwa ila za kukamatwa hawakuandika inaonekana gsm amewapa waandishi mpunga wa kutosha.

Tatizo la Simba ni media zake, website haitoi habari mara kwa mara na hata ikitoa ni nje ya muda, Twitter ni habari za mo na babra kidogo insta ndio wanajitahidi.

Simba wanatakiwa kutoa habari kupitia media zao lakini Manara, Hanspope, Babra, Kaduguda na viongozi wengine mara nyingi utawasikia mara wako wasafi, mwananchi, salehjembe badala ya kutumia vyombo vuao kutoa taarifa
 
Wanajihaaribia wao wenyewe na vipindi vyao vya michezo now wana msimbazi tutavisusia vipindi vyao uchwara ni siku izi nimejikuta spendi kuskilza michezo tena kama hapo nyuma naweza maliza wiki 2 hata 3 sjaskiliza ujinga ujinga wao maana mahaba kwa yanga yamekuwa makubwa sana au ndo senzo kawalipa!!?? Walichunguze hili aiseee
 
Unaumwa wewe unajua ku-buy media time hata kwa dk mbili tu ni bei gani?
Wanafanya hayo cause Simba fans ni pesa kwao ona sasa si mshaanza kuwazungumza hata wale wasiofatilia hayo mavipindi wataanza kufatilia wasikie nini chasemwa!

Na watawafuata hadi kwa social media zao mavyura yao yamelala tu
 
Wewe hata usikilize, husisikilize no impact wengine watasikiliza. Shida yetu ushabiki na mapenzi kwa timu yamezidi kuliko mchezo wenyewe, na hapo ndiyo soka letu lilipojikwaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…