Mchezo wa soka ni miongoni mwa michezo inayokusanya watu wa itikadi tofauti kabisa , mnaweza kuwa na makandokando yenu ya kisiasa lakini mkaja kukutana kwenye soka , kwa kifupi soka ni ya Wanamichezo .
Kitendo cha Yanga kumtangaza Mzee Kinana ambaye ni Kiongozi wa Juu wa CCM Kuwa mgeni rasmi wa siku yao waliyoipachika jina la SIKU YA WANANCHI , si tu kwamba hakikubaliki , Bali kinaleta sintofahamu kwa wale wana yanga ambao si wanaccm .
Mbona viongozi wa serikali ni wengi tu , kwanini aalikwe kiongozi wa ccm , Waalikaji wamelenga nini ?