hatutaweza kujua ni sababu gani iliyosababisha aachwe labda mpaka uongozi wa yanga uamue kuweka wazi sababu za kumuacha na uongozi haubanwi kuweka wazi sababu za uamuzi huo. labda kama mchezaji mwenyewe anajua sababu na akaamua kufunguka. kwangu mimi naona anatakiwa asikate tamaa kwani maisha ndivyo yalivyo afanye mazoezi bado uwezo anao na hata umri unamruhusu ila timu zinazomhitaji zimfanyie vipimo labda ana majeraha ya muda mrefu ambayo yamewatisha viongozi wa yanga. ajifunze kwa wachezaji wengine waliopitia matatizo kama yake, kwa mfano mohamed banka aliachwa na yanga akasajiliwa na simba akaja akacheza zaidi ya misimu 4 ya ligi kwa mafanikio na hata Idd Athumani Chuji alisajiliwa na simba akitokea yanga wakamkomoa wakamwacha akarudishwa yanga na kocha aliyewahi kumfundisha hapo hapo yanga (nimemsahau jina) akacheza takribani msimu 3 kwa kiwango cha juu.