Yanga yatozwa faini kwa mambo ya kijinga

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
Klabu ya Yanga imetozwa faini ya Sh 2,000,000 kwa kosa la mashabiki wake kurusha chupa za maji kiwanjani baada ya timu ya Ihefu kufunga bao la pili.

Pia kwa kosa la maofisa wa benchi la ufundi wa Yanga kuonekana wakipinga maamuzi na kumzonga mwamuzi wa akiba.
.
Naye Afisa Habari wa Yanga, Ali Kamwe ametozwa faini ya Sh 1,000,000 kwa kosa la kumkejeli na kumdhalilisha mwamuzi Malogo.
 
SHIRIKISHO la Soka Barani Afrika (CAF) limeipiga Klabu ya Simba faini ya dola za Kimarekani 10,000 zaidi ya Sh. Milioni 23.2 za Tanzania.

Adhabu hiyo imetokana na Simba kufanya vitendo vya kishirikina kwenye ya marudiano Robo Fainali Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji, Orlando Pirates Uwanja we Orlando Pirates Jijini Johannesburg, Afrika Kusini.

Simba ilitolewa kwa penalti 4-3 baada ya sare ya jumla ya 1-1, kila timu ikishinda 1-0 nyumbani.

Tayari Orlando Pirates imeingia Fainali baada ya kuitoa na Al Ahly Tripoli ya Libya kwa jumla ya mabao 2-1, ikishinda 2-0 ugenini na kufungwa 1-0 nyumbani.
 
Watamaliza ligi wako hoii...maana wakikaa nchale wakisimama nchale....
 

Akili ni nywere kila mtu anazake mkuu
 
Na marefa waliowabeba wamefungwa pia, ajabu unaleta habari nusunusu. Ngoja muone kama mtaendelea kubebwa. Nakuhakikishia mwisho wenu umefika.
 
Kule Simba kumejazwa mambumbumbu (in Rage's voice)
 
sema nyie wajinga zaidi,sijawahi ona wachezaji kuwasha moto kwa pitch aisee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…