Tetesi: Yannick Bangala avunja mkataba Azam FC, apishana kauli na Rached Taoussi

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Kiungo mkongwe Yannick Bangala amevunja mkataba na klabu ya Azam baada ya kupishana na kocha wake Rached Taoussi.

Bangala ambaye aliichezea Yanga misimu miwili kabla ya kutimkia Azam msimu uliopita tangu atimkie kwa matajiri hao wa Chamazi hajawa na rekodi nzuri kulinganisha na timu aliyotokea.

Katika misimu miwili aliyocheza Yanga alifanikiwa kufunga mabao matatu, huku Azam akifunga moja tu msimu uliopita, huku msimu huu akianza na majeraha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…