Yawezekana narudia uzi ila next move ya Feisal ni Simba SC

Kwasasa hana kiwango cha kucheza Yanga.

Yaliyowakuta hakina Domayo, Tshimbimbi, Gadiel, Nyonzima nk ajiandae naye kumkuta.
 
Yaani mpewe ndege kwenda na kurudi Algeria,mpewe mamilioni ya kodi zetu na ubwabwa wa ikulu halafu mlete fyoko fyoko fyoko !!!!
 
Kuna uzi nilishawahi kuupandisha humu kama sio kuuchangia, kuwa zile sarakasi za kipindi kile kuna wana walimchanua kuwa anatumika kidhuluma.,ila next move yake ilikua iwe Simba SC, Azam FC ilikua gharasha tu.

Na iwe na linakua.
Rais amekosea sana, na amekuwa biased, au kwasababu kile kidogo ni kizanzibari? faiza anachotakiwa kuelewa ni kwamba, siasa hazitamsaidia, mimi sijawahi kumkubali hata siku moja afu huwa naona hajui mpira.ndio maana hata nje hawezi kwenda kwasababu ya kichwa cha kamasi kama chake.
 
Yaani mpewe ndege kwenda na kurudi Algeria,mpewe mamilioni ya kodi zetu na ubwabwa wa ikulu halafu mlete fyoko fyoko fyoko !!!!
hiyo ndege sio ya Rais, ni ndege ya kwetu, halafu haya maamuzi ya mtu mmoja inabidi ifike mahali Tanzania tuyakatae. Katiba mpya ndio umuhimu wake nauona hapa, sasa hiyo ndege kwenda algeria na ni ndege ya biashara, ina maana Rais ametoa pesa kugarimia kibiashara au ameamuru tu kwamba ndege ambayo inatakiwa kuingiza pesa kibiashara iende huko? audit ya pesa hizo zinatoka wapi?za mtu binafsi, za taasisi? zinatoka kwa kifungu gani? au ukiwa Rais unaweza kutumia pesa yetu upendavyo?
 
Mbona mabango ya "ASANTE MAMA, 2025 ASIPINGWE" mliyajaza uwanjani, kama kweli mnapinga siasa michezoni mbona zilipokuja nyuzi za kuyapinga mliziponda, au kwakua mlikuwa wanufaika?

Tulieni siasa iamue.
 
Simba wajiangalie sana usajili wao.

No 10.

Clatus chama.
Saido Ntibazonkiza.
Moses phili.
FEISAL SALUM.


No 8.
Fabrice NGOMA.
Sadio Kanute

No6
Wajitahidi kupata kiungo mmoja WA ukabaji
 
Mbona mabango ya "ASANTE MAMA, 2025 ASIPINGWE" mliyajaza uwanjani, kama kweli mnapinga siasa michezoni mbona zilipokuja nyuzi za kuyapinga mliziponda, au kwakua mlikuwa wanufaika?

Tulieni siasa iamue.
ukweli mchungu ni kwamba, Rais hatakiwi kuingilia timu za mpira, kama anavyoonekana. kama mkataba unasema vingine na dogo anaonyesha kiburi, hatakiwi kutulazimisha kukubaliana naye, tutaweka mfano mbaya. na hapo mchezaji yeyote atakuja na mambo ya kiswahili ya kwenda kinyume na mkataba akijua kuna Rais atamtetea. ili michezo iende mbele hatuhitaji hawa wanasiasa waingilie kwa namna yeyote, na zaidi wengi wanaona anatetewa labda kwasababu ni mzanzibari. kiburi cha huyo dogi kisimchafue hata Rais na Rais ana mambo mengi na ya muhimu kuyafanya kuliko kufualia Faisal. tujifunze hata kwa marais wa nchi zingine tu kama wanaweza kuingilia mambo kama haya.

cha pili, mashirika ya ndege haya ni bora yakataifishwa tu yote, hata bandari taifisha hadi reli taifisha ili private sector ichukue mkondo wake. kukiwa na private sector iliyoshikilia hayo huwezi kuona malalamiko au doubts as to whether malipo yamefanywa au kiongozi fulani kaagiza ndege ipeleke lemutuz Dodoma, au ipeleke utopolo algeria. biashara gani hii? (kama amelipa pesa, Mungu ambariki, ila kama sio, tunaingiliwa wazee). hapo simba nao wanasubiri kuja kupewa ndege, Lipuli wanasubiri, azam wanasubiri, kwasababu ni cha wote, kila mmoja anatakiwa atendewe hivyo hivyo kwasababu umeanzisha. hii ndio sababu tunasema mashirika ya biashara hayatakiwi kusogelewa na wanasiasa kabisa.

pia, hivi kwa viongozi wanaoumiza kichwa kama Magufuli na wengine duniani, hata huo muda wa kufuatilia mpira unaupata wapi? ndio maana tunasema 2025 tunatakiwa kufanya maamuzi ya busara sana kwa ajili ya mwelekeo wa nchi yetu. we need to be more serious than we are now.
 
Simba wajiangalie sana usajili wao.

No 10.

Clatus chama.
Saido Ntibazonkiza.
Moses phili.
FEISAL SALUM.


No 8.
Fabrice NGOMA.
Sadio Kanute

No6
Wajitahidi kupata kiungo mmoja WA ukabaji
Kwa fabrice ngona nakataa,jamaa majeruhi sana.
 
Simba wajiangalie sana usajili wao.

No 10.

Clatus chama.
Saido Ntibazonkiza.
Moses phili.
FEISAL SALUM.


No 8.
Fabrice NGOMA.
Sadio Kanute

No6
Wajitahidi kupata kiungo mmoja WA ukabaji
ila usajili wa manzoki simba imepatia kiufupi tumelamba dume
 
faisal ameleta mfano mbaya sana kwa tasnia ya mpinga Tanzania. jeuri na kibri akijua ataonewa huruma. tutegemee wachezaji wengine wengi wakifuata mfano wake, na labda kwasababu sio wa kisiwani wanaweza wasipate mtetezi.
 
faisal ameleta mfano mbaya sana kwa tasnia ya mpinga Tanzania. jeuri na kibri akijua ataonewa huruma. tutegemee wachezaji wengine wengi wakifuata mfano wake, na labda kwasababu sio wa kisiwani wanaweza wasipate mtetezi.
Siku zote mla huliwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…