Yawezekana utapeli wa mtandao maarufu kama "tuma kwenye namba hii" ukawa unaratibiwa

Yawezekana utapeli wa mtandao maarufu kama "tuma kwenye namba hii" ukawa unaratibiwa

MKEHA

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
716
Reaction score
1,143
Habari wana JF,

Leo nimeanza kuamini kuwa wale jamaa wa TUMA KWA NAMBA HII ni matapeli walio kwenye ama makamouni ya simu ama mabenki yetu.

Leo nimetumiwa kiasi fulani cha fedha kwenye simu yangu. Aliyenitumia ametumia bank kuja kwenye mtandao wa simu.

Kabla hata sijamaliza kusoma ujumbe wa muamala huo zikaingia meseji tatu tofauti zote zikitaka kunitapeli kwa kunielekeza kuwa ile tuma kwenye namba hii.

Waliwezaje kujua kama kuna muamala simu yangu imeuapata kama sio organized crime?

Cha kushangaza nilikuwa na kama miezi mitatu siitumii simu yangu kwenye miamala lakini ghafla tu nimeanza kuitumia tayari na matapeli nao wameniona kuwa kiasi cha fedha kimeingia.

Tuishi kwa tahadhali kubwa enzi hizi za wizi wa mtandao. Tusitume fedha ovyo kwa watu tusiowajua na ikiwezekana mpigie simu mtu kabla ya kumtumia fedha ili kijiridhisha kama kweli ni mlengwa.
 
Hili hata mimi limenishangaza, nina namba ya simu ya mtandao fulani ambayo nimeimiliki huu ni karibia mwaka wa pili, na kimuamala wa pesa nimewahi kuitumia mara moja tu tena ni muda mrefu umepita, cha ajabu hii januari ndugu kanitumia 1k kupitia namba hiyo basi ghafla zikaanza kuingia SMS za miongozo kuwa nitume hiyo pesa katika namba gani, sasa najiuliza wanajuajeeeee! Kama kumeingia salio katika namba husikaaaa?

Pia kuna visms nimekuwa nikivipata kutoka katika namba za mtu binafsi akijifanya ni namba ya mtandao kuwa namba kadhaa ilikupigia muda fulani kwa hiyo wanakuwekea hiyo namba ili uipige mnh! hii nayo naona kama kamtego kengine kapya.

Anyway tunaishi dunia inayokwenda kwa kasi ya ajabu katika teknoloji, yatupasa kuwa na tahadhari ya kiwango cha juu mno.
 
Back
Top Bottom