Yaya Toure analalamika nini? Sio kila siku yeye, Aubameyang naye anastahili tuzo, eboh!

Yaya Toure kiwango kimepungua aache kulialia na kibaya zaidi mwaka 2015 alizidi kuchemka,huku kulalamika kunazidi kumshushia heshima
 
Kuuzwa mchezaji sio lazima kuisha kiwango kuna mambo mengi yanasababisha mchezaji kuuzwa huyo Aubemeyang wako kwa ligi km EPL au Laliga level ya timu kwake ni Malaga ,Swansea ama Southampton.
Umenena tima lake BVB lilikoswa koswa kushuka daraja
Wazungu wenyewe wanajua yaya ni nani
 
Mmesahau aliwahi kuinunia timu kisa hakupewa keki ya birthday. Huyu jamaa ni pwimpwi kweli.
 
Katukana wapi?? Yaya anasifa zifuatazo

Anakaba
Anafunga
Anatengeneza nafasi
Anaendesha team
Anashambulia

Na anasifa ya kuwa kiongozi bora kiwanjani.
 
Nimemdharau, pia ktk hii interview kuna mahali anakubali kuwa Messi anashinda trophies ila ronaldo anashinda ballon d'or, hiyo sababu ni ulaya anaona iko sawa! Hovyo kabisa, kashinda mara nne ila anaona wenzake hawastahili?
Alitaka avunje record,ndo maana kaumia sana maana angechukua mara tano yeye ndo angekuwa wa kwanza kufanya hivyo,anaona jamaa wamembania
 
Mmesahau aliwahi kuinunia timu kisa hakupewa keki ya birthday. Huyu jamaa ni pwimpwi kweli.
Keki na uwezo wa uwanjani wapi na wapi??

Watu wa mpira tanzania ni UOZO ULIOKUBUHU kwanzia mashabiki mpaka wachambuzi walio wengi ni baadhi tu ya wachambuzi ndo wapo sawa wengine ni mbute kabisa
 
Katukana wapi?? Yaya anasifa zifuatazo

Anakaba
Anafunga
Anatengeneza nafasi
Anaendesha team
Anashambulia

Na anasifa ya kuwa kiongozi bora kiwanjani.
Usijibu kwa kutumia historia ya miaka ya nyuma,Leta hizo statistics kati ya Toure na Auba za mwaka 2015
 
Kwani Aubemeyang kachukua mara ngapi?
Msimu uliopita Messi aliisaidia Barca kuchukua baadhi ya vikombe, ila ni ronaldo ndo alishinda Ballon d'or! Kwa fifa na europe ni sawa ila kwa afrika sio saw??
balon dor haitolewi kwa season year bali calendar year
 
Yaya alikuwanahodha kwenye timu ya taifa lakini alifunga goli moja na kutoa assist moja tu AFCON.
Baada ya michuano ile hajakuwa kwenye kiwango bora kwa mwaka mzima.

Tuzo ni ya mchezaji bora kwahiyo lazima ubora wa mchezaji udhihirike.

Spain walipotwaa kombe la dunia Xavi na Iniesta hawakupata tuzo ya mchezaji bora akaipata mchezaji mwenzao wa Barcelona, Messi.
 
Yaya toure kaonrwa that is openly seen... Tuzo hiyo ni ya mchezaji bora wa Africa 2015.., Toure aliisaidia timu ya taifa kubeba africa cup of nation
 
Huyu nae mbona anakuwa kama Ally Kiba!!! Kwann haamini kama wenzake wanaweza????? Mbona umri wake na vitu alivyoviongea ni tofaut?????
 
Unajua kuna vitu tunapaswa kuvichukulia kwa uzito wake ni ajabu Ivory coast miaka yote ina kamata mxhindi wa tatu na nne yaya anakuwa boora Afrika Leo nchi imekuwa bingwa chini ya Kapteni Yaya kwa mara ya kwanza kwenye CAF tournament af anapewa mtu mwingine ambaye hana lolote la kujivunia yy na bara hpn hii ni aibu kwa Afrika kuliko neno lenyewe aibu lilivyo shame on Hayatou na CAF yake kwa jumla.
 
...watu wamejaa ushabiki maandazi sana humu;haiwezekani Yaya ashinde kombe la mataifa ya Africa,halafu tuzo anakuja kupewa mtu mwingine kabisa ambaye timu yake ilitolewa kwenye hatua ya makundi?!,
borrussia dortmund hata champions league haipo!! this is utter nonsense!
Bora wangemwambia ukweli,bana wee umeshachukua sana hii tuzo,itapoteza mvuto, hebu waachie na wenzio angewaelewa...kuliko kufanya kituko kama hicho walichokifanya!
 
Yaya Toure amekuwa mchezaji bora mara nne na hakuwahi kuchukua ubingwa wa Africa mbona hao waliochukua ubingwa hawakulalamika?
 
Aubameyang 2015 ilikua chupu chupu ashuke daraja
Kuchukua ubingwa wa Africa sio benchmark ya kuwa mchezaji bora,Toure amekuwa mchezaji bora mara 4 mfululizo na hakuwahi kuchukua huo ubingwa wa Africa
 
Kuchukua ubingwa wa Africa sio benchmark ya kuwa mchezaji bora,Toure amekuwa mchezaji bora mara 4 mfululizo na hakuwahi kuchukua huo ubingwa wa Africa
...kumbe ubingwa wa Africa hauna maana! ndio maana wachezaji wengi wa nje huwa wanasingizia ugonjwa,ili wasije kujichosha huku!!
i see..!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…