benteke
JF-Expert Member
- Apr 3, 2014
- 1,305
- 1,068
Ah... nimekukumbuka kweli Yondo mpaka asubuhi wakati niko njiani nikaanza kucheka mwenyewe.... walikua wananiita Kanda bongo man na wewe walikuita Yondo sister... pale kijiji ilikua kunzia ubatizo, ubarikio, kipaimara na hata ndoa ilikua hatuachwi... walifikiria uhusiano wetu ulikua tu jukwaani kumbe hata nyuma ya jukwaa tulikua wapenzi.
Nilikua nikija tu kwenu mama akiniona tu kabla sijasema kitu basi alikua akikuita.... Yondooo... njoo huku mwenzio kaja kukuchukua muende mazoezi... mazoezi yenyewe hayakuishia kudansi tu. Nakumbuka sana ile staili ya mimi nakua kama naangalia juu ningeng'ata kidole kimoja na meno na huku kidole cha mkono mwingine kikiwa kinazunguka juu kama feni... wakati huo wewe ulikua unapita chini ya miiguu yangu... kwa kweli nimekukumbuka yondo.
Nasikia uko huku mjini na mambo yako ni mazuri sana.
Nilikua nikija tu kwenu mama akiniona tu kabla sijasema kitu basi alikua akikuita.... Yondooo... njoo huku mwenzio kaja kukuchukua muende mazoezi... mazoezi yenyewe hayakuishia kudansi tu. Nakumbuka sana ile staili ya mimi nakua kama naangalia juu ningeng'ata kidole kimoja na meno na huku kidole cha mkono mwingine kikiwa kinazunguka juu kama feni... wakati huo wewe ulikua unapita chini ya miiguu yangu... kwa kweli nimekukumbuka yondo.
Nasikia uko huku mjini na mambo yako ni mazuri sana.