Your Business is as Good as your team

Your Business is as Good as your team

Masokotz

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2018
Posts
3,713
Reaction score
6,121
Jaribu Kufikiri,

Umehangaika kutafuta business opportunity kwa njia unayoifahamu wewe,ukatafuta mtaji,ukaajiri wafanyakazi ili mfanye kazi pamoja mjenge kampuni,mjenge maisha.Ila Kila mara unajikuta unahisi kuna kitu unakikosa katika katika timu yako.Kuna wakati unafikiri labda hawana uzoefu au elimu au ujuzi wa kutosha.Kuna wakati unafikiri labda unawalipa kidogo sana au unawalipa kiasi kikubwa sana.Kuna wakatiunafikiri labda umekosea katika kuwaajiri.

Kuna mambo mengi sana ambayo unaona hayako sawa lakini bado unaona huna suluhu nayo.Unatengeneza Pesa na faida laini bado unaona kuna jambo haliko sawa.Hii ni moja kati ya changamoto ambayo wanapitia wafanyabiashara wengi wakubwa na wadogo.Swali la kujiuliza Je suluhisho yake nini?

Katika mazungumzo yangu marefu na mmoja wa wamiliki wa kampuni kubwa katika jiji la arusha ambaye naye anapitia changamoto kama hiyo niligundua tatizo ambalo linaweza kuwa chanzo cha hii changamoto.

Wajasiriamali wengi na wamiliki ya biashara hufanya makosa katika kuajiri wafanyakazi wao.Wengi wao husahau kwamba wafanyakazi wao nao ni watu ambao nao wana maono,malengo na mataraji katika maisha yao na kwamba wanapokuja katika kampuni au biashara yako wanataraji waweze kufikia malengo yako kupitia fursa unayowapa.Huwa wanasahau pia kwamba unapoajiri mtu basi lazima uwe na hakika majukumu yake yatakuwa ni yapi na yawe wazi na ya hakika na sio kuajiri mtu kwa ajili ya kujaza nafasi katika ofisi yako.

Wajasiriamali wengi huona raha kwamba watu wanaripoti ofisini mapema hata kama hakuna kazi za kufanya na wanakaa ofisi siku nzima hata kama hawana cha maana wanachofanya.Tunapoajiri tunanunua muda wa mtu ingawa hatuuhitaji muda huo.Tunasahau kwamba ajira sio muda tu bali ni zile skills za mtu ni sehemu ya ajira na ni lazima ufahamu namna ya kuzitumia.

Lengo la kuleta mjadala huu ni kutaka kujadili mbinu ambazo unaweza kuzitumia kujenga timu ya wafanya kazi wake na kuifanya iwe na tija kwako na kwenye biashara yako.Je utazame vigezo gani wakati wa kuamua nani umuajiri?Ni vigezo vya msingi vya kuzingatia katika kufanya uamuzi wa ni nani aajiriwe katika kampuni yako na kwa nafasi gani?

Karibu tujadiliane
 
Kujenga timu bora inahitaji.
1. Walipe vizuri

2. Washikishe malengo ya kampuni, wajione ni sehemu ya kampuni.

3. Waheshimu, omba ushauri kwao inapo idi.

4. Wape mafunzo. Trainings za soft skills, Digital, Sales, marketing Nk.

5. Pamoja na kuwa ni wafanyakazi lakini fahamu ni binadamu

6. Kujenga timu bora mpe kila mtu majukumu yake, Fanya waamini wanaweza kutatua tatizo bila kulifikisha juu.

IG @kelvinkibenje
 
Kujenga timu bora inahitaji.
1. Walipe vizuri
Assumption: Wako productive. Unawalipa kwanza ili wawe productive au wawe productive kwanza ndio uwalipe vizuri? Chicken and egg...!
Kuwalipa vizuri ndio inakuwaje? Ni fedha tu au na mazingira ya kazi? Ain't that simple, is it?

2. Washikishe malengo ya kampuni, wajione ni sehemu ya kampuni.
Ulimaanisha washirikishe? If that is the case, then I agree. Maono ya kampuni yanapaswa kuwa so deep entrenched kwa kila employee. Lakini kama anafanya kazi kwa sababu ya (1) then hana haja ya kujua maono kivile. Anakuwa anaishi sio kusukuma maono per se bali anafanya kazi zake zamwezi huu ili ATM isome!

3. Waheshimu, omba ushauri kwao inapo idi.
Waheshu kweli, Ndio sura ya biashara kwa wateja. Ila kama hawajiheshimu hii itafeli tu!
Utaomba ushauri kama wana value ya kuongeza au cha kushauri. Kama ni vilaza kuomba ushauri ni suicidal mission!

4. Wape mafunzo. Trainings za soft skills, Digital, Sales, marketing Nk.
Hii ni kama wana mpango wa kukaa. Unagharimika na mafunzo unawanoa wakiwa kwenye shape bora, wanasepa kwenye dau kubwa zaidi.
5. Pamoja na kuwa ni wafanyakazi lakini fahamu ni binadamu
Kweli kabisa, na kuna binadamu wa tabia nyingi tofauti, nzuri na mbaya!

6. Kujenga timu bora mpe kila mtu majukumu yake, Fanya waamini wanaweza kutatua tatizo bila kulifikisha juu.
Kuweka majukumu wazi (Clear delegation of authority) ni jambo muhimu. Niongeze tu unapowapangia majukumu lazima uwape mamlaka ya kutekeleza majukumu hayo. Ila tena kumwamini mtu asiye makini na mamlaka ni tatizo, atayatumia malaka vibaya tu!

Ninachojaribu kusema ni hiki: Hatua ya kwanza kujenga timu ni kupata watu sahihi ambao watakuwa watafuta sio kijiwe cha kupatia mia mbili mia tatu, bali sehemu ambayo wanataka kuwekeza moyo wao na ujuzi wao, ili kuungana na mwajiri kujenga anachotaka kujenga. Kwao hawa malipo ni compensation tu ya wao kuwa sehemu ya ujenzi wa maono.

Hawa kuwapata duniani, sio kazi rahisi. Hawa kuwapata Bongland, ni mziki mnene!
Ila ukiwapata, hatua tajwa inakuwa rahisi kwenda nazo japo sio mteremko kama inavyoonekana!

IG @kelvinkibenje
IG @adiuta_biz 😉
 
Assumption: Wako productive. Unawalipa kwanza ili wawe productive au wawe productive kwanza ndio uwalipe vizuri? Chicken and egg...!
Kuwalipa vizuri ndio inakuwaje? Ni fedha tu au na mazingira ya kazi? Ain't that simple, is it?

IG @adiuta_biz 😉
Shukrani sana
 
Back
Top Bottom