Yuko wapi director Mtitu g game film?

sir venance

Senior Member
Joined
Oct 26, 2017
Posts
151
Reaction score
223
Huyu jamaa ni moja kati ya watu wasioongelewa kabisa hapa nchini hususani katika tasnia ya filamu za kibongo,japokuwa wengi wetu filamu za kitanzania zimetutoka kabisa mioyoni mwetu,ila kuna watu Kama Mtitu game au Gabriel Mtitu walikua ndio watu waliotengeza filamu nzuri za kibongo hapo nyuma,huyu kupitia kampuni yake ndio aliowaibua wakina marehemu Steven kanumba,Ray,johari, Irene uwoya nk., asilimia 70 au 80 za movie za kanumba zilikua zinaongozwa na director huyu,movies Kama johari,Oprah,nk zote ziliongozwa na huyu jamaa,lakini cjawahi ona hata media yoyote kufanya interview na Mtitu game hii ni kutothamini mchango wake,kwa wanaomfahamu vizuri huyu jamaa bado yupo kweli?
 
Dah kweli huyu jamaa alitoa muvi nzuri sana zilizotamba miaka hio. Nimefaidi sana muvi zake kwenye mabasi katika safari zangu za boarding.
 
Yani ilikuwaga nikiona tu yale matangazo yake ya game 1st quality tz limited Basi huwa naamini hakuna movie atakayokosea chini ya usimamizi wake.
 
Yupo mbona bado ana direct. .ila tamthilia kama ile ya jirani na mama kubwa
 
Movie gani hizo za kuiga. Eti........A Mutitu Game Film Presents Oprah.......yaani kwa kuwa Filam za Nigeria zinaanza na ......An Obierika Movies Presents Arrogant Husband ....na Mbongo naye anaanza hivyo hivyo !!!
 
Movie gani hizo za kuiga. Eti........A Mutitu Game Film Presents Oprah.......yaani kwa kuwa Filam za Nigeria zinaanza na ......An Obierika Movies Presents Arrogant Husband ....na Mbongo naye anaanza hivyo hivyo !!!
Halaf huyo ndio muanzilishi wa" NGE NGE NGE" kila mwanzo wa mshtuko katika bongo muvi
 
Movie gani hizo za kuiga. Eti........A Mutitu Game Film Presents Oprah.......yaani kwa kuwa Filam za Nigeria zinaanza na ......An Obierika Movies Presents Arrogant Husband ....na Mbongo naye anaanza hivyo hivyo !!!

We fala kweli , hizo ni film convention ulimwengu mzima, acha upuuzi
 
We fala kweli , hizo ni film convention ulimwengu mzima, acha upuuzi
Ni kweli mimi naweza kuwa Fala, lakini sio FALA kuliko wewe ? Wewe ndio Kiongozi wetu Mafala, maana kila siku huwa unaanzisha Thread za kufuatilia maisha ya watu. Aidha, sina chuki na mtu yeyote kama wewe ulivyo na chuki na watu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…