Yupo wapi jf member BAK ?

Lile jamaa siku likitokea ntalipa tuzo ya msimamo usioyumba wakiume kama jamaa wa zile kinikia. Jf nzima ndio linamiliki konsitensi ya kusimamia upinzani tangu enzi za kikwere.
 
Aliyumba lkn aliyumbia mwelekeo uleule. Kama alikuwa hasi akawa hasi mbili. Ila wewe nae unajitahidi kukomaa na chama dola.
2015 iliyumbisha wengi sana humu jamvini na ikawapotezea confidence na credibility
 
alipoteza msimamo 2015
mkuu 2015 hata mimi niliaibika sana kwenye mtaa. Yaani nililazimika kumpigia kura LOWASSA sio kwa sababu ni Bora au Magufuli hafai ila kwa sababu kwangu CCM haijawahi kufaa.

nilijivunjia heshima, na sasa sitaki kabisa mambo ya kisiasa maana mission yangu ya kushiriki kuangusha mbuyu kwa njia ya lowassa ilifeli. nilipoteza hadi marafiki.

hiyo 2015 tumsahemehe tu, maana hata sisiem mlikuwa namalalamiko ya majina ya mifukoni.
Ila jamaa BAK limeiwekea hazina JF tangu 2008 na mabandiko reliable yenye mlengo wa kuikosoa serikali.
 
Huyo atakuwa kala BAN ya kimya kimya kufuatia maagizo kutoka mamlaka za juu... Na huenda JF waliamriwa wampige ban ya kimya kimya ili JF iruhusiwe kurudi hewani.
 
Nimempima BAK na wanaJF wengi kwa kipimo cha uzalendo na dhamira za kuibadilisha nchi nimemuona hatoshi.
JF ya zamani niliiamini imekaa kizalendo kwa maana ya members wake kuchangia kwa style ya kuibadilisha nchi.Ila mwaka 2015 niligundua kuwa wengi wao walikuwa ni members wanasiasa waliokuwa wanajijenga kisiasa tu.Hawakuwa na msimamo wa kizalendo.
Hawakuwa tayari kumkosoa yoyote anayekosea awe ndani ya CCM au nje ya CCM..Kumbe walikuwa kiitikadi zaidi.ndio maana Magufuli alipopitishwa baadhi yao walibadili misimamo au kuamua kukaa kimya.
Mimi niliamua kubakia kama mzalendo na mwenye kusimamia misimamo ya kizalendo ...of course kwa sasa itikadi ,sera na misimamo ya CCM imelenga kwenye uzalendo ndio maana nipo huko !
Ikitokea CCM ikafanya au ikarudia madudu yake ni lazima nitaibadilikia vilivyo!
Tupo hapa kutoa maoni yetu kwa ajili ya kuijenga nchi !
Jf kwa upande wake imesimama hivyo kama forum ndio maana kuna kipindi wanaCCM wanailaumu na wapinzani wanailaumu na huwa inavumilia.Ndio maana naiombea iwepo milele.
Kwa sasa nitasimama na CCM adilifu no matter what hadi perception yangu itakaponiambia kuwa CCM imeachana na misingi ya uadilifu.
 
Asante mkuu. Ila CCM ni ileile kuitofautisha hii na ile nikujitafutia bp. Ngoja tuitafutie Kodi tutajaji vzr 2025
 
Asante mkuu. Ila CCM ni ileile kuitofautisha hii na ile nikujitafutia bp. Ngoja tuitafutie Kodi tutajaji vzr 2025
CCM Kamwe sio ile ile...hii ni CCM ya Magufuli na kila mwanaCCM anaelewa hili
 
CCM Kamwe sio ile ile...hii ni CCM ya Magufuli na kila mwanaCCM anaelewa hili
Ule wimbo ccm ni ileile muufute mkuu. Maana Sasa hivi kila anayetsjwa kwenye ripoti za kifisadi ananyea ndoo kupitia mahakama ya mafisadi
 
CCM Kamwe sio ile ile...hii ni CCM ya Magufuli na kila mwanaCCM anaelewa hili
Ule wimbo ccm ni ileile muufute mkuu. Maana Sasa hivi kila anayetsjwa kwenye ripoti za kifisadi ananyea ndoo kupitia mahakama ya mafisadi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…