Yupo X-road!

Jaguar

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2011
Posts
3,437
Reaction score
1,027
Nimepata shuhuda ya barua ya dada mmoja kupitia redio fulani ya kidini.Huyu dada ana watoto watatu,mtoto wa pili kazaa nje ya ndoa,mumewe hajagundua na anampenda mno huyu mtoto wa pili kuliko hata wale wengine wawili ambao ndo wa kwake halali.Huyu dada kaokoka na sasa ni mcha mungu.Kuna kitu kinamweka njiapanda,je..amwambie mumewe ukweli wa yeye kuzaa nje ya ndoa au aifanye siri mpaka kifo chake?Hivi sasa anaishi maisha ya raha mustarehe na mumewe mpenzi,mwanamke ameokoka na anataka kujivua gamba,aanze maisha mapya masafi ya kumpendeza mungu,mpeni ushauri.
 

nina wasiwasi,baba anaweza asiwe baba wa kunizaa..dah, kweli anayejua mzazi wa mtoto ni mama

Mi nadhani sidhani kama anahitaji kuweka wazi wakati huu ambao ndoa ndio tamu..Atulie tu, labda kama haipendi ndoa..
 
Pole zake huyo dada mana hii issue. Inabidi achague nani zaidi mhimu kwake. The Husband au God. Cause kama kweli anamtaka the husband kumwambia its really out of question, sidhani kama the husband ataelewa mana ataanza kutia wasiwasi hata kwa hao wake kweli. Na kama ameokoka inamhitaji amwamble the husband ukweli cause God ataona wokovu wake kutokamilika kwa kukaa na siri kubwa kama hiyo bila kuambia the husband. she has to choose, The Lord Or the Husband then she will know what to do.
 
kama biological father hajui kuhusu huyo mtoto anaweza akafa na hiyo siri japo kibinadamu ni ngumu sana haswa akifikia umri wa baadae sana pale huyo mtoto akiwa mtu mzima atapata tamaa ya kumweleza ukweli,

kama biological baba analijua hili ni bora aseme mapema maana kuna siku atakuja ku-claim mtoto wake....better later than ever sababu akisema mapema yaweza ku-affect pia makuzi ya huyu mtoto haswa kwa baba wa kufikia...
 
akae kimya hadi atakapoamua KUOKOKA ...bado anaigiza tu.
 
Wokovu wa kweli hauhofii mabaya, so hawezi kuficha dhambi kuuuubwa kiasi hicho, Jesus bado hajatua moyoni.
Zaburi ya 23 iwe taa kwake. Abarikiwe.
 
Huyo mama asirogwe kumwambia mmewe,inahusu? yeye si wa kwanza wala wa mwisho kuzaa nje ya ndoa,mkemia mkuu alisema vipimo vya DNA vimeonyesha 50% ya watoto wanazaliwa na baba chanja,usichokijua ni usiku wa giza na mbwa aliyelala usimwamshe.Maumivu ya kusema 'ukweli' hayataishia kwa baba tu yatahamia kwa mtoto na madhara yake ni mabaya sana,'kitanda hakizai haramu'!
 
Kwa faida ya mtoto simshauri aseme. Atamwathiri huyo mtoto sana. Vile baba mlezi hajagundua,aendelee kubaki na siri yake, afanye maombi na atubu sana, na asirudie tena!
 
Kwa faida ya mtoto simshauri aseme. Atamwathiri huyo mtoto sana. Vile baba mlezi hajagundua,aendelee kubaki na siri yake, afanye maombi na atubu sana, na asirudie tena!
Ushauri mzuri S.L,lakini kwa sisi wakristo mtu unatakiwa kutubu,kujuta na kuacha dhambi na baada ya hapo kama ulimkosea mtu,unatakiwa kumfuata kumwomba msamaha ili usamehewe na MUNGU juu mbinguni na wanadamu duniani.Huyu dada ameokoka na kumpokea yesu kristo kama mwokozi wake,anataka kujivua gamba na kuachana na asili chafu ya zamani na kuanza maisha mapya.Mungu anasema maombi ya mtu mwovu ni kelele masikioni mwangu na sadaka ya mtu mwovu ni machukizo mbele ya macho yangu.Kwa hiyo kama akiamua kuficha siri basi aachane na mambo ya uokovu na akae na asili yake ya uovu mpaka kifo chake for the better of her son!
 
Acheni masihara, kwanza huyo mwanamke ni mpumbavu kwanini asingemweleza huyo mwanaume ukweli kabla hawajazama deep katika mapenzi?
Na hakuna siri itakayodumu dunia hii.
Anaonesha kabisa ni mwongo, mnafiki, haina haja yakuokoka. Madhara ya huo ujinga ni makubwa kuliko angesema mwanzo na huyo mwanaume kama anaakili,busara na uelewa wa maisha atamuelewa na wataishi kwa furaha. Rejea filamu ya "THE LOST TWINS" by mtitu game.
 
Kwanza hajaokoka ,au hajui maana ya kuokoka .Ndoa kitu gani mbele za Mungu adadavue kila kitu Kwani kwa Mungu hakuna kinachoshindikana
 
Point taken!
 
Hapo ndio najiuliza wanawake wengine sijui wanawazaje? wewe unajua kabisa unacheat na umeolewa, halafu unapata mimba then unaamua kuzaa, huo ni uuwaji kabisa, unajua huyo baba anaweza asimuache lakini akafa kwa presha. Yaani hadi kuzaa? ili umuoneshe huyo unaecheat nae kwamba unampenda sana au? wanawake wengine bana. haya sasa linywe hili, na kama umeokoka kutoa ushuhuda muhimu, hapo ndipo pagumu
 
Bora mie copy n paste hakuna hata haja ya DNA
 
mi najua ni mtoto wa baba yangu, na mwanangu ni mtoto wangu...
huyo mama ni bonge la nyoka, mwache aendelee kuficha af mume aje agundue mwenyewe atakiona cha moto jinsi ghadhabu za kudanganywa mda mref zinavyokuwa
 
Kutubu tunatubu kwa Mungu na anayetusamehe ni Mungu....kuokoka hakusemi kawatangazie binadamu uliowakosea madhambi yako...pangekalika hapa duniani? dada ametambua makosa yake,katubu na kamrudia Mungu yatosha....na aziache njia zake mbaya....!!

Wote tuna dhambi nyingi tu,kwanini muone kwamba yeye kukosea kuzaa nje ya ndoa ni zaidi ya yule anamuacha mumewe ndani au mkewe for whatever reasons na kwenda nje?

Aombe hekima ya Mungu na amsome mumewe zaidi....kama ni mtu anayeweza kubeba hili amuambie,kama sio na iwe siri yake hadi kifo au atakapokuwa na sababu ya kukiri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…