Yutong/zongtong/Higer and scania buses

yutong,zutong NEW FORCE HANA MPINZANI KWASASA HAPA EAST AFRICA NA ATATEKA HADI AFRICA YOTE
Teh teh teh new force hana mpinzani EAST africa? Unachokiongea unakijua? Eti atateka africa yote? How? Ushafika hata hapo msumbiji tu ukamuona huyo mtu wa shinyanga anaitwa NAGI NAGI, achana na huyo unamjua MANING NICE vizuri achana na gari zake za dar mtwara naongelea zile za nampula-maputo, maputo - luanda etc....huko anajiita Tanga raha. Achana kuzungumza ya hovyo hovyo bwana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hapa umeongea, kuna watu wanaponda utafikiri wameshawai kufanya hata bishara ya daladala
 
Uko sahihi kabisa. Scania kwa ubora inaongoza. Lakini kwa tabia za abiria heri kununua mabasi ya kichina kwa sababu abiria wa sasa wanaangali namba za magari. Wakiona ina series za C... hawapandi wanataka D.. tena kwa sasa DK... Sasa ukinunua scania kwa bei ghali ukitazania likae miaka 5 utapanda wewe mmiliki na familia yako tu ingawa litakuwa bado jipya.
 
Ishu ni bei tu, yutongo, higer, zhong tong zinakaa njiani kwa dola 150000 pamoja na import duty, vat, railway levy. Scania yenye body ya marcopolo, Irizar ni kuanzia dola 250000 na kuendelea before tax.
 
Kwa kawaida wafanyabishara wanaangalia mizania ya faida kabla ya izo mambo zingine ndo maana utaona baadhi ya magari yanaondoka yenyewe barabarani bila kufukuzwa, kwa mfano unaona ujio wa mitsubish fuso canter inakuja used kutoka japan inavuliwa bodi inajengwa bodi ya tandam inabeba tani hadi 12 kutoka tani 4 za awali gari hiyo ikipakia mzigo sawa na mzigo ulipakia kwenye scania purling(kipisi) kwa safari moja mfano dar-arusha wakati scania ianakula lita 180+ iyo fuso inakula 100 au chini ya hizo that means margin ya faida inaibeba iyo fuso kuliko hiyo scania hapo bado hujaangalia bei ya spea na bei ya gari yenyewe, ukija kwenye scania verses yutong ndio kabisaa kwanza ni matajri wachache huku kwetu wanamudu kununua scania mpya kwa hiyo taste ya scania buses ziliziko bongo nyingi ni old fashioned kwa hiyo taste yake iko chini kwa abiria ambapo ukiangalia yutong peke yake brand za sasa zipo too modern yani gari inavutia . ukija kwenye ulaji wa mafuta ndi balaa kabisa wataalamu wanadai umbali ambao scania inaenda kwa lita za dizeli 100 yutong inaweza kwenda kwa lita 75-80 , kwa mwendo ndio usiseme sasa utaona kiufupi huku kwetu scania itakimbia kama zilivyokimbia nissan diezel na isuzu achilia mbali leyland daf na leyland comet , isuzu na ford ambazo sasa zishakuwa wahenga.
 
Ishu ni bei tu, yutongo, higer, zhong tong zinakaa njiani kwa dola 150000 pamoja na import duty, vat, railway levy. Scania yenye body ya marcopolo, Irizar ni kuanzia dola 250000 na kuendelea before tax.
Mkuu, unajua Dola 150,000 ni sawa na kiasi gani?
 
Salehe Nagi au Nagi Nagi yule jamaa anatisha pale Msumbiji huyo mtu SHY ni shida ana bus kama mia tatu ziko yard acha zinazotembea
 
Pia gari za kichina body zake ndio zinauza ubungo na kokote pia zikichoka engine huwa wanazibadilisha wanafunga engine ya scania na gear box ya scania inaendelea kupiga mzigo kama kawa ndio maana soko la scania linapotea ila yutong au zongtong linazidi kukua huku kwetu sababu zina option mbili ikichoka engine unabadilisha
 
Bado angalia Mechanics Scania zipo juu lakini pia ina mudu umbali mrefu mfano mtu unaleta Yutong Dar to Kigoma unategemea nn sasa kingine gharama Scania Moja unapata Yutong mbili hata kama mimi ntanunua sababu cheap
 
Nilichogundua Bus zenye injini ya Scania ni imara sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…