Zaburi tuliyosomeshwa na Halima Mdee hai-support kabisa

Zaburi tuliyosomeshwa na Halima Mdee hai-support kabisa

El Roi

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2020
Posts
297
Reaction score
537
Nianze kwa kukiri kwamba nilifurahishwa kiasi kumuona Halima akitueleza vile mama yake alivyompa neno la faraja kutoka kitabu cha zaburi 35 katika masaibu yake.

Ni tabia njema upande m moja kuona Watu wanakimbilia msaada wa vitabu vitakatifu kwa ajili ya faraja au hata kupata ufumbuzi wa shida zao. Hapa nampongeza Halima kwa kukumbuka maandiko.

Tatizo tu ninaloliona ni kama hiyo zaburi inaendana na matatizo yake ya sasa.

Kwa sisi ambao kiasi tunafuatilia mafundisho ya kidini, mara zote huwambiwa kwamba" maandiko huwa yana asili yake na aina yake ya kutafsiri. Alichofanya Halima ingawa kanukuu maandiko lakini yako nje ya maana(out of context).

Mtunga zaburi anaposema Mungu apigane na wanaopigana naye, hana maana Mungu apigane vyovyote(blindly) bali mtunga zaburi hapo, kama mtu mwenye haki (Righteous) anataka Mungu awe upande wake!

Kumbuka Mungu huwa upande na wenye haki.

Je, wakati Halima anajifariji kwa hiyo zaburi, ni kweli roho yake inamshuhudia kuwa mwenye haki ktk sakata lake? Maana kujifariji kwa maandiko wakati roho yako inakushuhudia vinginevyo ni faraja hewa.

Nakubaliana na alichosema mchungaji Msigwa mahali fulani kwamba, Halima na wenzake wanapaswa kutubu maana " dhambi iliyotubiwa haina nguvu tena" badala ya kujifariji kwa maandiko.

Ni vizuri kujifariji kwa maandiko lakini in right motive and not in wrong motive.

Utapata amani sana Halima na wenzako endapo utatubu ulivyofanya kinyume na order na taratibu zenu badala ya kupata faraja ya maandiko ambayo hayakutii moyo kuishi bila order. Kujifariji kwa maandiko wakati mzizi wa dhambi umefichwa ni kutafuta amani ya bandia ambayo haitakusaidia kwa hakika.

Wasalaam.
 
Nilitegemea Huyo Halima nukuu yake aitoe kwenye Quran lakini navyojua Zaburi inapatikana kwenye biblia.

Kwa nukuu hii huenda Halima ni mkristo.
Hongera Halima kwa kumkumbuka Mungu

Imani ni bora kuliko Dini.
 
Ndiyo! Hawa mabeberu wa chama hawakutaka kuwapa uheshimiwa kina mama bila kuwavua chiup***.
Kina mama wakaamua kupigania haki yao huku wakilinda utu wao.
Tuna kila sababu ya kuwa support hata kama sisi hatuko huko kwenye iko charma!
 
Nilitegemea Huyo Halima nukuu yake aitoe kwenye Quran lakini navyojua Zaburi inapatikana kwenye biblia.

Kwa nukuu hii huenda Halima ni mkristo.
Hongera Halima kwa kumkumbuka Mungu

Imani ni bora kuliko Dini.
Ulivyoona jina Halima ukajua ni muislam?
Jina sio dini
Kalagabaho
 
Zaburi ya 137 ingefaa sana kumfariji.
Zaburi 137 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹ Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi, Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.
² Katika miti iliyo katikati yake Tulivitundika vinubi vyetu.
³ Maana huko waliotuchukua mateka Walitaka tuwaimbie; Na waliotuonea walitaka furaha; Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.
⁴ Tuuimbeje wimbo wa Bwana Katika nchi ya ugeni?
⁵ Ee Yerusalemu, nikikusahau wewe, Mkono wangu wa kuume na usahau.
⁶ Ulimi wangu na ugandamane Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka. Nisipoikuza Yerusalemu Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu.
⁷ Ee Bwana, uwakumbuke wana wa Edomu, Siku ya Yerusalemu. Waliosema, Bomoeni! Bomoeni hata misingini!
⁸ Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia, Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.
⁹ Heri yeye atakayewakamata wadogo wako, Na kuwaseta wao juu ya mwamba.
 
Zaburi 137 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹ Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi, Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.
² Katika miti iliyo katikati yake Tulivitundika vinubi vyetu.
³ Maana huko waliotuchukua mateka Walitaka tuwaimbie; Na waliotuonea walitaka furaha; Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.
⁴ Tuuimbeje wimbo wa Bwana Katika nchi ya ugeni?
⁵ Ee Yerusalemu, nikikusahau wewe, Mkono wangu wa kuume na usahau.
⁶ Ulimi wangu na ugandamane Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka. Nisipoikuza Yerusalemu Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu.
⁷ Ee Bwana, uwakumbuke wana wa Edomu, Siku ya Yerusalemu. Waliosema, Bomoeni! Bomoeni hata misingini!
⁸ Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia, Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.
⁹ Heri yeye atakayewakamata wadogo wako, Na kuwaseta wao juu ya mwamba.
Kweli kabisa, Mdee ilitakiwa a dedicate zaburi hiyo
 
Back
Top Bottom