Zacharia Hans Pope baada ya Yanga kuchukua Ubingwa wa VPL

Headline Yako Umeandika " Kauli Ya Ltd Captain Zacharia Hans pope Baada Ya Yanga Kuchukua Ubingwa Wa VPL ". Naomba Kujua Hiyo Abbreviation Ya Ltd Inamaanisha Nini? Nitashukuru Ukinielimisha Kuhusiana Na Hilo Mkuu Kwani Humu Tunajifunza Pia!

Mkuu ndo mana nikamaliza "Ni mimi tu kuwaletea habari".. Nimeileta kama nilivyoipokea.
 
Headline Yako Umeandika " Kauli Ya Ltd Captain Zacharia Hans pope Baada Ya Yanga Kuchukua Ubingwa Wa VPL ". Naomba Kujua Hiyo Abbreviation Ya Ltd Inamaanisha Nini? Nitashukuru Ukinielimisha Kuhusiana Na Hilo Mkuu Kwani Humu Tunajifunza Pia!

Nadhani alimaanisha Rtd (Retired) na siyo Ltd (Limited). Huenda naye ni Msukuma kama mimi maana kule kwetu penye 'R' huwa tunaweka 'L' and vice versa. Huo ni utamaduni wetu (wala usicheke) kama kwa ndugu zetu Wachagga panapo 'nchi' huweka 'nji'
 
Hata mla mgonjwa anaeharisha, hujiliwaza kula KANDE kuwa eti anafunga choo. Wakati, anajimaliza na kuongeza, matatizo. Hivi kuna ujenzi unaendelea hapo?

kwa team inayojiendesha kwa kuwakopa wachezaji wake mishahara..unajenga labda msingi wa biscuit
 
Nadhani alimaanisha Rtd (Retired) na siyo Ltd (Limited). Huenda naye ni Msukuma kama mimi maana kule kwetu penye 'R' huwa tunaweka 'L' and vice versa. Huo ni utamaduni wetu (wala usicheke) kama kwa ndugu zetu Wachagga panapo 'nchi' huweka 'nji'

Nakuheshimu Wewe Na Nakupenda Kwa Vitu Vikubwa Viwili Tu. Kwanza Hiyo Picha Ya Ktk AVATAR Yako Na Pili Uwezo Wako Wa Kujibu Hoja Na Upeo. Hakika Unaitendea Haki Mno Hiyo Picha Uliyoiweka Ktk AVATAR Yako Na Ningeshangaa Kama Na Wewe Usingekuwa Na Uwezo Mkubwa Wa Kufikiri Kama Wa Huyo Uliyemweka Pichani. Ubarikiwe Sana Kwa Kuiweka Hiyo Picha Mkuu Na Nafurahi Sana. Akhsante Kwa UFAFANUZI Wako Wa Kina Na Nimeelewa Sasa!
 
Mikia bhana, tabu sana. Iwe Yanga au Simba lazima tukubali kwamba hamna aliyewahi kuchukua kombe lolote la CAF. Being almost a man is not being a man per se.

Waliotoka Dar kwenda Kigoma mmoja akaishia Morogoro na mwingine akaishia Tabora, wote wana sifa moja - hawajafika Kigoma.

Pamoja na hayo nashukuru Makoye Matale kaweka data ili watu walinganishe ndio waseme. Ubingwa wa Bongo Yanga kachukua mara 24 na mikia mara 17. Hilo pengo mbona Hans Pope mhaini halisemi? Msamaha ufutwe arudi jela kunyea debe.

Hivi kiongozi wa Mikia ni Aveva au Hans Pope?
 

Championship update: Yanga 25-17 Simba.
 
Ameacha kutafuta namna ya kulipa maden ya akina tambwe na logarusic pamoja na hela ya kuiendesha timu yao yeye anakuwa busy kuizungumzia yanga!!!!

Simba haina bahati ya viongoz.......

Mkuu, huyo popo wala si kiongozi. Bahati kawakuta waliochaguliwa wapo wapo tu anafanya anavyotaka. Kiongozi wa kikamati awe na sauti namna hiyo?

Uhaini unamzuia kikatiba kugombea uongozi. Atabakia kwenye vikamati fake.
 
huyu H.P juzi alikuwa akikalamika madeni, njaa na hali ngumu kwenye timu, leo anakuja na porojo zingine... hapo ndo nayakubali maneno ya rage.
 

sasa mbona mlifukuza makocha na wachezaji mkidai kuwa hawaisaidii timu kushinda ili mchukue ubingwa..wakati lengo lenu sio ubingwa???
 
Nadhani alimaanisha Rtd (Retired) na siyo Ltd (Limited). Huenda naye ni Msukuma kama mimi maana kule kwetu penye 'R' huwa tunaweka 'L' and vice versa. Huo ni utamaduni wetu (wala usicheke) kama kwa ndugu zetu Wachagga panapo 'nchi' huweka 'nji'

Nkoi Makoye nene nale msukuma, fomu yane Ntobho Kahama, o wewe fomu yakho mahe?
 
sasa mbona mlifukuza makocha na wachezaji mkidai kuwa hawaisaidii timu kushinda ili mchukue ubingwa..wakati lengo lenu sio ubingwa???

Lengo la kutimuliwa ilikua ni kujenga timu, ubingwa ni matokeo.
 

Wanamakombe mangapi ya kimataifa hawa mikia? au ameamua kuwafurahisha mashabiki wa mikia fc kwakuwa wanategemea tena kuishia nafasi ya tatu, wakiitwa mambumbu wanachukia, huyo jamaa kaonesha ukomavu wa umbumbu wake, kumbe halafu wanaandaa timu kwa msimu ujao sasa wanalilia nafas ya pili ya nini? msimu huu wenyewe walikuwa wakishnda wanasema ndio wameanza ligi, wakifungwa wanasema timu bado changa kuna wachezaji wadogo wadogo.
 
sasa mbona mlifukuza makocha na wachezaji mkidai kuwa hawaisaidii timu kushinda ili mchukue ubingwa..wakati lengo lenu sio ubingwa???

lengo lao ni kusindikiza mabingwa ili wachukue ubingwa
 
sasa mbona mlifukuza makocha na wachezaji mkidai kuwa hawaisaidii timu kushinda ili mchukue ubingwa..wakati lengo lenu sio ubingwa???

lengo la mikia ni kusindikiza mabingwa ili wachukue ubingwa
 

Mbona Ktk Simba Uwekundu Wa Mafanikio UMETAWALA Lakini Upande Wa Yanga Uwekundu Wa Mafaniko Ni Wa Kuhesabu? Simba Oyeee!
 
Kwa hiyo unataka kusemaje?

Angalia Mafanikio Hapo Juu Kisha Nyie Wana Yanga Ndiyo Mjilinganishe Kwa Mafanikio. Wenzenu Simba Tunaenda Na Data / Facts Kama Hizo Ulizowekewa Hapo Ili Kuwadhihirishieni Kuwa Wana Simba Ni Wasomi WALIOTUKUKA Na TUNAJUA TUNACHOKIFANYA Na TUNA MAFANIKIO YA KIMATAIFA YALIYOTUKUKA! Kama Unapingana Na Hizo Data Hapo Si Mbaya Na Wewe Ukatuwekea Zako. Yanga Mashabiki Kibao Lakini Wasomi Hawazidi Hata 10 Sasa Njoo Kwa MNYAMA. Yaani Nyie Kote Kote Sisi Simba Tunawazidi. Na Hapo Bado Hujawekea Na Data Za " SUPER OKWINYO " Alivyoitesa Yanga Mara Zote Alizoichezea Simba!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…