Zahanati Mpya Kufunguliwa Leo Kijijini Nyabaengere, Kata ya Musanja

Zahanati Mpya Kufunguliwa Leo Kijijini Nyabaengere, Kata ya Musanja

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

ZAHANATI MPYA KUFUNGULIWA LEO KIJIJINI NYABAENGERE, KATA YA MUSANJA

Utoaji wa Huduma za Afya waendelea kuboreshwa ndani ya vijiji vya Jimbo la Musoma Vijijini.

Kata ya Musanja yenye vijiji vitatu (Mabuimerafuru, Musanja na Nyabaengere) haikuwa na zahanati hata moja - wanatembea umbali mrefu kwenda kupata Huduma za Afya kwenye Kata jirani ya Murangi

Vijiji viwili (Nyabaengere na Mabuimerafuru) vinajenga zahanati za vijiji vyao, na leo Kijiji cha Nyabaengere kinazindua utoaji na Huduma za Afya kwenye zahanati yake mpya.

Michango ya ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Nyabaengere:

(i) ujenzi ulianza kupitia Harambee ya Mbunge wa Jimbo kwa kukusanya michango na nguvu kazi za wanakijiji na viongozi wao

Mbunge wa Jimbo: saruji mifuko 100

Diwani na Wanakijiji: thamani ya michango yao ni takribani Tsh milioni 5 (Tsh 5m)

Wazaliwa wa Kijiji cha Nyabaengere wamechangia jumla ya Tsh 400,000 (laki nne)

(ii) baadae, Halmashauri yetu (Musoma DC ilichangia Tsh milioni 50 (Tsh 50m)

(iii) vilevile, Serikali Kuu ilichangia Tsh milioni 50 (Tsh 50m)

Huduma za Afya zinaanza kutolewa leo, na ukamilishaji wa ujenzi wa miundombinu inayohitajika unaendelea.

Picha iliyoambatanishwa hapa:
Jengo la Zahanati ya Kijiji cha Nyabaengere

SHUKRANI:
Wananchi ya Jimbo la Musoma Vijijini na viongozi wao wanaendelea kuishukuru Serikali yetu inayoongozwa vizuri na Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuchangia fedha nyingi za utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya vijijini mwetu (Musoma Vijijini)

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

P.O. Box 6
Musoma

Tarehe:
Ijumaa, 6 Dec 2024
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2024-12-06 at 12.27.24.jpeg
    WhatsApp Image 2024-12-06 at 12.27.24.jpeg
    59.6 KB · Views: 6
Back
Top Bottom