Zaidi ya ekari elfu 7 za mazao ya wananchi Kigoma zavunwa na watu wasiojulikana na nyumba kuchomwa

Zaidi ya ekari elfu 7 za mazao ya wananchi Kigoma zavunwa na watu wasiojulikana na nyumba kuchomwa

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
nyumba%2811%29.jpg

Wananchi wa kijiji cha Kitanga katika wilaya ya Kasulu mkoani kigoma wamelalamika zaidi ya ekari elfu saba za mazao kuvunwa na watu wasiojulikana pamoja na nyumba zao kuchomwa kutokana na mgogoro uliosababisha pia kifo cha mtu mmoja.

Wamemwambia Naibu waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi,kumekuwa na mgogoro wa shamba hilo ambalo linamilikiwa na halmashauri ya wilaya kwa muda mrefu kati ya wafugaji na wakulima ambapo hivi karibuni mazao yaliyolimwa na wananchi mbalimbali yalivunwa usiku.

Naibu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Mh.Dk. Angelina Mabula ameagiza kuchukuliwa hatua kwa watu waliofanya uhalifu, huku mkurugenzi wa Halmashauri Godfrey Kasekenya akiahidi kushughulikia mgogoro huo.

Chanzo: ITV

PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
Duh! Hii hatari sasa. Hii migogoro viongozi si wapo wanashindwa nini kutafuta suluhu?!
Hii nchi kazi ipo...
 
Ekari elfu 7 kuvunwa usiku na watu wasiojulikana jamani huu ni uongo kweupeeee. Ekari elfu 7?

Sent from my TECNO-L8 using JamiiForums mobile app
 
Duh! Hii kali watu wanavuna hekari saba bila hata mtu kuwafahamu.
Mkuu soma vizuri sio ekari 7 ni ekari 7000. Ni jambo lisilowezekana kwa hata kwa wiki moja labda use combine harvester za kutosha.

Sent from my TECNO DP8D using JamiiForums mobile app
 
Mkuu soma vizuri sio ekari 7 ni ekari 7000. Ni jambo lisilowezekana kwa hata kwa wiki moja labda use combine harvester za kutosha.

Sent from my TECNO DP8D using JamiiForums mobile app
Shukrani mkuu ni katika uandishi nimekosea maana nilikuwa najua nimedelete hiyo post. Ni jambo ambalo haliwezekani...
 
Maajabu ya dunia hao watu walikuwa wana vuna time gani

Sent from my TECNO Camon CX using JamiiForums mobile app
 
Hii inadhihirisha kuwa uchawi Tz umeadvannce hadi kuunda combine harvesters

Sent from my Infinix_X521 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu soma vizuri sio ekari 7 ni ekari 7000. Ni jambo lisilowezekana kwa hata kwa wiki moja labda use combine harvester za kutosha.

Sent from my TECNO DP8D using JamiiForums mobile app

Inawezekana ni wala rambirambi hao tukakague kule wanakotoa buku saba saba!
 
Wanalaumu nini, wakati wao ndio walio ruhusu warundi kuvuka mipaka na kuishi pamoja nao....[emoji45] [emoji45] Mbaya zaidi ni pale mamlaka zinapo jaribu kuwakamata, wamekua wakisingizia kwamba wao ni wakazi wa maeneo hayo
 
Back
Top Bottom