Zaidi ya Wananchi Laki moja Ngorongoro, wadaiwa kupangiwa maeneo ya kupigia kura ambako sio wakazi

Zaidi ya Wananchi Laki moja Ngorongoro, wadaiwa kupangiwa maeneo ya kupigia kura ambako sio wakazi

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
276
Reaction score
473
Wananchi zaidi ya Laki moja wadaiwa kukosa haki yao ya msingi ya kupiga kura katika maeneo yao ndani ya Tarafa ya Ngorongoro Wilayani Ngorongoro badala yake inaelezwa kwamba wengine kwa mujibu wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), wamepangiwa kupigia kura Msomera mkoani Tanga licha ya kutokuwa wakazi wa huko.

Wakizungumza Agosti 2,2024 mbele ya waandishi wa habari mkoani Arusha, waliojitambulisha kuwa wawakilishi wa wananchi hao wamedai kuwa wamesikitishwa na kitendo cha kunyimwa haki ya kupiga kura katika vituo vyao vilivyopo katika Tarafa ya Ngorongoro.

Akizungumzia hilo Dwani wa kata ya Oloitole iliyopo Tarafa ya Ngorongoro, James Moringe amesema kuwa amesikitiswa kwa uamuzi huo wa kunyimwa haki kupiga kura maeneo ya Ngorongoro na badala yake kupangiwa kupiga kura Kijiji cha Msomera mkoa wa Tanga wakati bado hawajahamia huko kwa hiari kama Serikali inavyodai.

Ameongeza kuwa wao kama Wananchi wa Tarafa ya Ngorongoro wanailaumu Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kwa kuondoa vituo vyao vya kupigia kura katika chaguzi badala yake kupeleka majina yao katika Tarafa zingine na Msomera bila hiari yao.

Aidha Mwenyekiti wa Kijiji cha Bulati, Sabore Ngarus amesema kuwa wao ni wawakilishi wa wananchi wa tarafa ya Ngorongoro ambao wanadai haki yao ya kupiga kura katika maeneo yao wanayoishi.

Amesema kufuatia orodha ya vituo vya kujiandikishia kupiga kura Nchi nzima iliyotolewa na INEC imeviondoa vituo vya kujiandikisha kupiga kura katika Kata kumi na moja (11) na vijiji ishirini na tano (25) ndani ya Tarafa ya Ngorongoro badala yake anadai wamepangiwa kujiandikisha katika Tarafa zingine pamoja na Msomera.

Bwana Sabore amebainisha kuwa tume imefanya kinyume na taratibu na ibara namba tano (5) ya tume huru ya uchaguzi ambayo inampa kila mtanzania haki ya kuchagua na kuchaguliwa.

Itakumbukwa Serikali kupitia kauli za vingongozi mbalimbali ikiwemo Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na vingozi wengine wamekuwa wakisikika kuwa wananchi katika eneo hilo wanaohama wanaondoka kwa hiari na kuwa wanaobaki hawalazimishwi kuhama.

Soma: Serikali yafuta vijiji na vitongoji vyote vya wamasai wa Ngorongoro kupitia Amri ya tangazo la Serikali namba 673

Lakini kumekuwepo na mwendelezo wa taarifa zinazodai kuwa baadhi ya huduma zimekuwa zikisitishwa kwa wakazi waliobakia eneo hilo kinyume na ilivyokuwa awali kabla mchakato wa kuhama haujaanza.

Pia Soma
~ Wamasai wa Ngorongoro watoa tamko kunyang'anywa haki ya kupiga kura 2024 na 2025
~ Njama: Vituo vyote vya kupigia kura Jimbo la Ngorongoro vimefutwa, ila watu bado wapo na Jimbo bado lipo
 
Mimi ninachojua Kodi yangu imetumika kuwajengea nyumba Msomera na kuhamishwa Bure wenyewe na mifugo yao.
 
Watanzania mmeamua kukaa kimya bila kuwasemea ndugu zenu Ngorongoro , Vyombo vya habari hasa mainstream media tv, redio na magazeti mmeamua kukubaliana kutokutoa taarifa za watanzania hawa, viongozi wa dini mmeamua kufumbia macho zambi hii , wanasiasa na vyama vya siasa hamuoni kama kuna watu wanaaumia sana Tarafa ya Ngorongoro, wadau wa maendeleo mmejikausha kana kwamba hamjui nini kinaendelea Tarafa ya Ngorongoro, viongozi wastaafu mengine mtasema ila la Ngorongoro sio tatizo kwenu,

Viongozi wa sasa hamna huruma na watu hawa, Wasomi nchi waliishia enzi za Kina Shivji, Asasi za kiraia mmevaa miwani za mbao.

Kwa ufupi mmeamua kututupa na kututenga watu wa Tarafa ya Ngorongoro. Hakuna shida tutabaki na roho zetu na Mungu wetu. Nyie mko salama kwa sasa. Lakini nawakumbusha hakuna makali yasiyokuwa na ncha na hakuna myonge asiyekuwa na Mtetezi. Mungu atafanya njia. Walisema ni hiari , wakaanza kunyima huduma za msingi za jamii lakini jamii ikaendelea kuishi kwa kumtegemea Mungu na sasa Tarafa nzima sawa na nusu ya wilaya ya Ngorongoro haipo kwenye mchakato wa kuandikishwa kama wapiga kura wa Ngorongoro.

Hadi vyombo vya uchaguzi navyo vimeingia katika mkakati wa kuhakikisha tuna kosa haki zetu zote Tarafa ya Ngorongoro. Kumbukeni katiba ya Tanzania inasema Ibara ya 21 na Ibara ya 5.-(1) Kila raia wa Tanzania aliyetimiza umri wa miaka kumi na minane anayo haki ya kupiga kura katika uchaguzi unaofaywa Tanzania na wananchi.

Na haki hii itatumiwa kwa kufuata masharti ya ibara ndogo ya (2) pamoja na masharti mengineyo ya Katiba hii na ya Sheria inayotumika nchini Tanzania kuhusu mambo ya uchaguzi.Kuchagua na kuchaguliwa ni haki ya kila mtu.

Lakini sasa kama walivyokosa haki zingine wanakwenda kukosa haki hii kinyume na Katiba. Ni kosa gani tumefanya watu wa Ngorongoro hata kustahili ghadhabu hii?
 
Katika mambo ambayo serikali inakosea kwa jina la uwekezaji ni kuhamisha wazawa wa eneo asilia na kuwapeleka makazi ambayo yako tofauti na ekolojia yao. Hili ni bomu na ipo siku litaripuka tu haijalishi muda gani utapita
 
Kwa nini mambo haya hayawekwi wazi? Kwa nini Tume Huru ya Uchaguzi haisemi kitu kuhusu Jimbo hili la Ngorongoro?
 
Duh wanataka ngorongoro iwe nyeupe wasiwepo wamasai

Ova
 
CCM na serikali yake wameamua kuuza Tanganyika kwa reja reja, tukija kustuka hakutakuwa na nchi Tanganyika bali mapori ya Waarabu!
 
Wananchi zaidi ya Laki moja wadaiwa kukosa haki yao ya msingi ya kupiga kura katika maeneo yao ndani ya Tarafa ya Ngorongoro Wilayani Ngorongoro badala yake inaelezwa kwamba wengine kwa mujibu wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), wamepangiwa kupigia kura Msomera mkoani Tanga licha ya kutokuwa wakazi wa huko.

Wakizungumza Agosti 2,2024 mbele ya waandishi wa habari mkoani Arusha, waliojitambulisha kuwa wawakilishi wa wananchi hao wamedai kuwa wamesikitishwa na kitendo cha kunyimwa haki ya kupiga kura katika vituo vyao vilivyopo katika Tarafa ya Ngorongoro.

Akizungumzia hilo Dwani wa kata ya Oloitole iliyopo Tarafa ya Ngorongoro, James Moringe amesema kuwa amesikitiswa kwa uamuzi huo wa kunyimwa haki kupiga kura maeneo ya Ngorongoro na badala yake kupangiwa kupiga kura Kijiji cha Msomera mkoa wa Tanga wakati bado hawajahamia huko kwa hiari kama Serikali inavyodai.

Ameongeza kuwa wao kama Wananchi wa Tarafa ya Ngorongoro wanailaumu Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kwa kuondoa vituo vyao vya kupigia kura katika chaguzi badala yake kupeleka majina yao katika Tarafa zingine na Msomera bila hiari yao.

Aidha Mwenyekiti wa Kijiji cha Bulati, Sabore Ngarus amesema kuwa wao ni wawakilishi wa wananchi wa tarafa ya Ngorongoro ambao wanadai haki yao ya kupiga kura katika maeneo yao wanayoishi.

Amesema kufuatia orodha ya vituo vya kujiandikishia kupiga kura Nchi nzima iliyotolewa na INEC imeviondoa vituo vya kujiandikisha kupiga kura katika Kata kumi na moja (11) na vijiji ishirini na tano (25) ndani ya Tarafa ya Ngorongoro badala yake anadai wamepangiwa kujiandikisha katika Tarafa zingine pamoja na Msomera.

Bwana Sabore amebainisha kuwa tume imefanya kinyume na taratibu na ibara namba tano (5) ya tume huru ya uchaguzi ambayo inampa kila mtanzania haki ya kuchagua na kuchaguliwa.

Itakumbukwa Serikali kupitia kauli za vingongozi mbalimbali ikiwemo Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na vingozi wengine wamekuwa wakisikika kuwa wananchi katika eneo hilo wanaohama wanaondoka kwa hiari na kuwa wanaobaki hawalazimishwi kuhama.

Lakini kumekuwepo na mwendelezo wa taarifa zinazodai kuwa baadhi ya huduma zimekuwa zikisitishwa kwa wakazi waliobakia eneo hilo kinyume na ilivyokuwa awali kabla mchakato wa kuhama haujaanza.

Pia Soma
~ Wamasai wa Ngorongoro watoa tamko kunyang'anywa haki ya kupiga kura 2024 na 2025
~ Njama: Vituo vyote vya kupigia kura Jimbo la Ngorongoro vimefutwa, ila watu bado wapo na Jimbo bado lipo
Nia yao ni kuwafanya wasipige kura kwa kuwa wanajua ni anti-CCM.CCM ni janga nchini kwetu kwa kweli,they are so irrational and uncouth.
 
Mimi ninachojua Kodi yangu imetumika kuwajengea nyumba Msomera na kuhamishwa Bure wenyewe na mifugo yao.
Kodi yako? Bunge lipi iliidhinisha bajeti ya matumizi ya kodi yako?
Ipo siku utajua zilikotoka yale mabilioni.
 
Nia yao ni kuwafanya wasipige kura kwa kuwa wanajua ni anti-CCM.CCM ni janga nchini kwetu kwa kweli,they are so irrational and uncouth.
Ni zaidi ya hivyo... Najua unajua. ccm haitegemei sanduku la kura kushinda uchaguzi.
Hapa sababu ya msingi ni kuwaongezea Masai shinikizo ili waendelee kuhamia Msomera kwa "hiyari".

Wajanja wanataka ardhi... Juu waweke hotels, chini wachimbe madini!
 
Kumbe wamasai wana ONGEA kiswahili vizuri tu, inakuwaje hawa tunaopishana nao humu mjini wanaongea kiswahili mbofu mbofu?
 
Kwa wengi Kiswahili ni lugha ya pili au ya tatu.
Waliozungumza wote wame ONGEA kiswahili vizuri kabisa, hadi nikashindwa kuelewa, hawa tunaopishana nao humu mjini wao kwanini wanaongea kiswahili mbofu mbofu.
 
Back
Top Bottom