Zakia Meghji na uuzaji wa Mbuga zetu je atapeta pia ?

Kibunango na kundi lako nadhani hamkuwa mna elewa nataka nini .Unajua ukiwa umejiandaa kubisha kila kitu kwa ushabiki unakuwa mpuuzi na hata huwezi kuelewa maandiko.Wale walio nielewa nawashukuru na tuendelee kukata nyeti hapa .Wengine walikuwa watoto waodogo sasa mambo haya ni historia kwao .Meghji ni mmoja wa watu walio lihujumu sana Taifa letu .Mimi najiuliza kwa nini hajawahi kusimama jimboni akaomba kura kila mara ana teuliwa na kupewa uwaziri ? Huyu mama si ndiye kwa pamoja na Ngosongwa walidai kwamba we can use a US$ bila ya matatizo badala ya shiling Bungeni ?

Bado nataka kujua zaidi kwa walio nadata zaidi .Je anaenda hivi hivi kweli wakati kaliangamiza Taifa ? Again I insist on kunyoosha rekodi .
 
Kibunango na kundi lako nadhani hamkuwa mna elewa nataka nini .Unajua ukiwa umejiandaa kubisha kila kitu kwa ushabiki unakuwa mpuuzi na hata huwezi kuelewa maandiko.

Umetaja Loliondo na kumhusisha Meghji na hilo, Kukmbukumbu zinaonyesha kuwa kipindi hicho waziri wa Utalii alikuwa ni A. Mgamia na kutokana na hilo alijiuzuru uwaziri wake...

Sasa futa kwanza kauli ya Loliondo na Meghji ili tuweze kujadili otherwise ni majungu katika kupikwa. Na zaidi ni upuuzi kuja na mada za kizushi hapa
 
kuna daktari mmoja hivi wa mazingira kule morogoro(nikipata jibu nitawaambia
)

DR KIRAHAMA SASA HIVI YUKO WIZARANI NI MKURUGENZI WIZARA YA MALIASILI UPANDE WA MISITU KAMA SIKOSEI
 

Kibunango
hivi hii kashfa ya Abubakar mgumia ni tofauti na ile iliyoibuliwa kuhusu Loliondo ikamfanya Dr.Juma Ngasongwa ajiuzulu?Nakumbuka kujiuzulu kwake kipindi cha mkapa ilimhusisha kumuuzia mwana wa mfalme wa nchi za kiarabu kipande cha mbuga.
 
Kibunango
hivi hii kashfa ya Abubakar mgumia ni tofauti na ile iliyoibuliwa kuhusu Loliondo ikamfanya Dr.Juma Ngasongwa ajiuzulu?Nakumbuka kujiuzulu kwake kipindi cha mkapa ilimhusisha kumuuzia mwana wa mfalme wa nchi za kiarabu kipande cha mbuga.
Dr. J Ngasongwa alijiuzuru uwaziri wa Utalii mwaka 1996 na baada kasi ya skandali ya loliondo na issue nyingine huko kwenye mbuga za wanyama kuongezeka aidha hakutiwa hatiani katika kushiriki kwenye skandali hiyo na ndio maana Mkapa akampa wizara nyingine baada ya kujiuzuru kwake.

Meghji aliingia kwa mara ya kwanza kwenye wizara hiyo mwaka 1997 ikiwa ni zaidi ya miaka mnne baada ya skandali ya Loliondo kuiburiwa
 
Last edited:
Dr. J Ngasongwa alijiuzuru uwaziri wa Utalii mwaka 1996 na baada kasi ya skandali ya loliondo kuongezeka aidha hakutiwa hatiani katika kushiriki kwenye skandali hiyo na ndio maana Mkapa akampa wizara nyingine baada ya kujiuzuru kwake

Mkuu Kibunango
Hebu jaribu kucheki vizuri rekodi zako, sijui zangu ndiyo zitakuwa na makosa ama zako ndiyo zitakuwa na makosa maana hapa hatugombani ila tunawekana sawa katika kupata ukweli.

Rekodi yangu inaonyesha Bi. Zakia Hamdani Meghji amekuwa waziri kwa kipindi hiki:
1994 -2005: (Minister) Ministry of Natural Resources & Tourism
2006 - 8/2/2008: (Minister) Ministry of Finance

kwa hiyo nachanganyikiwa kidogo unaposema Dr. J. Ngasongwa alijiuzuru uwaziri wa utalii mwaka 1996: wakati mwaka 1996 kwa rekodi zangu tayari wizara ilikuwa mikononi mwa Mama Meghji.

Tuendelee!
 
Mkuu Kibunango

Rekodi yangu inaonyesha Bi. Zakia Hamdani Meghji amekuwa waziri kwa kipindi hiki:
1994 -2005: (Minister) Ministry of Natural Resources & Tourism
2006 - 8/2/2008: (Minister) Ministry of Finance

Tuendelee!
Z. Meghji alianza uwaziri katika wizara ya Afya kama sikosei na tokea hapo akaenda Utalii kabla ya kuwa waziri wa Fedha..
  • 1995 - 97 : Waziri wa Afya
  • 1997 - 2006: Waziri wa Utalii
  • 2006 - 2008: Waziri wa Fedha
 
Savimbi huyu mama kaingia wizara ya MALI YA ASILI 1997.
kIPINDI CHA RUKSA alikuwa wizara ya Afya.
Ila kakaa kwa mda mrefu wizara ya mali asili
 

Kweli vichekesho,sasa hizi ndo data zilizoombwa kuhusu uuzaji wa mbuga zetu au masihala?
 
Kuna haja ya kuulizia hao ambao wanahusika na ukusanyaji na uandikaji wa CV za Wabunge wetu... Kwani hii hapo juu ni upotoshaji mkubwa wa habari na ni uzembe wa hali ya juu kwa asasi hiyo muhumi(Ofisi ya Bunge).
 
Last edited:
Ukitaka kashfa nyingine ya Zakia Meghji ni katika ubinafsishaji wa uwanja wa ndege wa Kilimanjaro(KIA) kwa bei ya kutupa na Zakia Meghji ndiye aliyesaini mkataba huo(Waziri mwenye dhamana),mbaya zaidi kwa bei ya kutupa;Zitto alivyosikitishwa na mkataba huo akaomba copy;Zakia akajibu mkataba ni siri.
Taarifa zaidi ingia jubi.wordpress.com halafu upande wa mkono wako wa kulia juu (pages) halafu ka-click maneno yafuatayo,"KWA MPANGO HUU UMASKINI LAZIMA."
 
Kiuyajibu toa ufafanuzi alisaini mkataba wa ubinafsishaji wa Uwanja wa ndege wa KIA akiwa waziri mwenye Dhamana ktk Wizara ipi,kwani viwanja vya ndege vyote viko chini ya wizara ya ujenzi na wizara ya mawasiliano na je Zakia Meghji alishawahi kuwa waziri katika wizara hizo?
Jamani tuje na evidence na masuala ya uhakika na si kusema alisaini mkataba au alifanya hiki.Hizo ni here say ambazo si mzuri kwa wana JF.
Kazi njema
 
kibunango,savimbi,ham,kiuyajibu...

..Juma Ngasongwa alijatwa ktk ripoti ya Warioba kwamba alihusika na suala la Loliondo wakati akiwa mshauri wa uchumi wa Raisi Ally Mwinyi.

..Kwasababu hiyo akajiuzulu ili kumpa nafasi Raisi Mkapa achunguze suala hilo.

..Inaelekea Mkapa aliona kwamba Ngasongwa alitajwa kimakosa hivyo baadaye akamrudisha kwenye baraza la mawaziri.

..Kuna waziri m-Zanzibari anaitwa Juma Hamad Omar ambaye ali-serve wakati wa Raisi Mwinyi. Huyu naye alifanya hujuma kubwa sana ktk Wizara ile. Ilifika mahali mpaka wabunge wakawasilisha hoja binafsi kupinga uharamia wa Juma Hamadi Omar.

..Pia mchunguze vitimbi vya Muhidin Ndolanga wakati akiwa Mkurugenzi wa Wanyama Pori.

..Abubakar Mgumia[r.i.p] alikuwa mtu safi. aliondolewa pale kwasababu alikuwa akibabaika ktk kutetea ufisadi wa Loliondo mbele ya wabunge.

..Baada ya kuondolewa Mgumia akateuliwa Juma Hamad Omar ambaye aliweza kusimamia na kutetea hujuma zilizokuwa zikiendelea.

NB:

..Wizara ya Maliasili na Utalii si Wizara ya Muungano lakini Wazanzibari wamekuwa wakiteuliwa kuongoza Wizara hiyo. Hilo lililamikiwa hata ktk hoja ya Tanganyika.


+
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…