Zama zako zikipita kubali kuacha wenye zama zao wafurahie

Mwanasayansi Kalivubha

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2024
Posts
344
Reaction score
926
ZAMA ZAKO ZIKIPITA KUBALI KUACHIA WENYE ZAMA ZAO WAFURAHIE😊

Mambo uliyotakiwa ufanye ukiwa na miaka 10 ukiyafanya leo una miaka 30 Utaonekana kituko 😊

Na usipokubali umri wako ukaanza kujirudisha nyuma kwa kufanya mambo ya kupingana na umri wako pia utaonekana kituko na kibaya zaidi utakuwa unapoteza muda.


Umri ukikupita huwezi kuurudisha nyumba bali ukubali tu kuwa sasa unatakiwa ufanye mambo ya kuendana na umru husika kwa mfano ukiwa na miaka 45 akili kubwa ifikirie utaishije uzeeni kipindi ambacho utakuwa na nguvu ya kula ila huna nguvu ya kufanya kazi.

Umri ni kama zama tu zikipita ndio basi tena kubali kuhamia kwenye zama nyingine na usianze kuona wivu kwa walio kwenye zama zao.


Kuna ambao umri bado unawaruhusu kufanya mambo fulani na kuna wengine tayari umri umeshakuwa kikwazo ila unaweza kulazimisha tu uonekane kituko na mtu wa ajabu mwenye kupoteza muda .

Kubali tu kuwa sasa wewe wa miaka 40 siyo yule tena wa miaka 20 na ukiweza hilo utafurahia sana maisha 😊

#Mwanasayansi Saul kalivubha
#fikia ndoto zako.
 
Shida ni Kwann Uziache ,Inabidi usiruke stage
Kabisa😎
 
Uzi makini sana huu
 

Hii picha utakuwa ulishawahi kuiona kwenye memes sana, huyu mzee anaitwa Flavio Briatore ni mfanya biashara tajiri mkubwa huko Italy, amezeeka na mwili wake haupo kwenye shape nzuri, lakini jamaa anafahamika kwa kuwachakata wadada warembo kweli kweli wengine maarufu ambao ni models.







Mzee anawachakata vyema na amefumaniwa na paparazi mara kadhaa akiwa na warembo wabichi kabisa akiponda raha sehemu mbali mbali.

Mtu akiwa na pesa, uzee haupo.
 
 
Madada ndiyo hawakubali kama muda wao umepita ,unamkuda mmama ana zaidi ya miaka 40 lakini bado anavaa majinsi ya kubana ,vitop ,kujikwatu na mikucha ,mikope etc wakati hayo mambo ni ya watoto wa 20's
 
Dah!
Pesa sabuni ya roho.
 
Masikini tu ndiyo huwa tuna hii ishu ya rika ila hauwezi mkuta tajiri anaandika haya 😁😁😁
 
Ila ukiwa na pesa mambo yanaweza kuwa tofauti kidogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…