Tetesi: Zamu ya Muhongo kuumbuka

Prof.Muhongo unamuonea ndugu! Tumuache afanye kazi majungu hayalisaidii taifa kwa sasa. Ebu fikiria kidogo, kabla muhongo hajaingia barazani ufisadi haukuwepo? Weka wazi na ushahidi wako wapi muhongo anahusika kwenye wizi ?
 
MUHONGO ITAKUWA KASHATUMBUA MTU AU KAZIBA MRIJA WA MTU,UKISIKIA WIIIIIIIIIIIIIII UJUE KIMEMPATA HUYO.
 
Hivi Magu alikuwa na ajenda gani kumrudisha huyo Muhongo aliyekataliwa na wananchi? The most arrogant figure, corrupt and a liar, rejected by wananchi bungeni akajuizulu then akarudishwa nafasi ile ile. Shamefull. Now according to the karma laws, the most affected person is the one who went against wishes of the majority souls. He will eventually axe him but he will have proved to himself that he has actually became a surgeon of his own boil. (jipu). This will prove to him that he is not serious sometimes. According to his philosophy he will have contradicted himself in deed, hence psychological effect. kwa kiswahili ni kwamba atajisikia kujitumbua mwenyewe kwa hiyo atapata mfadhaiko, roho itamsuta kwa kutosikliza sauti wa wengi a.k.a sauti ya Mungu..
 
Nakumbuka ilipotoka habari ya sefue kuwa jipu mlikuja juu humu ndani,mkasema sio kweli,anazushiwa,baadaye nini kilitokea???
Hivi kuna watanzania wenzetu kabisaa hawaoni madudu ya prof.Muhongo!!?,iweje yeye tu atajwe kila kona?
Je,ni kwamba hapendwi?anaonewa?au anatenda madudu hayo kweli?
Mimi nadhani uchunguzi ufanyike pasipo kumbeba wala kumuonea yeyote,ikiwa anafanya mambo ya hovyo kama inavyozungumzwa,asionewe haya hata kidogo,ATUMBULIWE TU!!!
 
MUHONGO ITAKUWA KASHATUMBUA MTU AU KAZIBA MRIJA WA MTU,UKISIKIA WIIIIIIIIIIIIIII UJUE KIMEMPATA HUYO.
Kwa taarifa yako muhongo hana uwezo wa kutumbua mtu . Labda wale wafagiaji wa pale wizarani na watu wadogo wadogo. Hutaki? Kaulize!
 
Sipingani na mawazo yako mkuu. Tusubiri tuone ndio unihukumu.
 
Unaona mercenaries wake wanavyonishambulia na wengine kunitusi? Subiri mkuu! Mark my words and my post.
 
Nyie wafanyakazi wa wizara ya madini mlizoea vya kunyonga,ssa vya kuchinja hamviwezi;mlizoea mzaha mzaha kazini,sasa Muhongo ndo kiboko yenu.
Dada jambo usilolijua ni kama usiku kwa giza nene.
Naomba nishie tu hapa maana hutanielewa. Ila muda ndio wakati muafaka.
 
Reactions: MTK
Hizi ni chuki tu..ikiwq kama mtaendeleza fitina na majungu ya kijinga tu na kutishia watu eti watumbuliwe huo ni ujuha tu...ulichoandika hapo hakuna issue ni majungu ya kuzoazoa tu
 
Kumrejesha Muongo kulikuwa ni kosa la kiufundi tangia mwanzo! Huwezi kumfundisha Simba mzee mbinu mpya za kuwinda! That guy is egocentric and arrogant by gene formation, hawezi kubadilika!
 
Mkuu Muhongo ni Jembe hasa kwa sisi Wateja wa Tanesco! Jaribu kuangalia muda mfupi alioshika simbachawene linganisha na Sasa, Mnaomchukia huyu jamaa ni Mameja,wafanyakazi na wapiga dili wa madini na Tanesco, Lakini watasubiri sana na haitatokea kirahisi kama wanavyotaka wao. Muhongo piga kazi{Hapa kazi tu}.[emoji109] [emoji3]
 
Ukipewa kusimamia wodi ya vichaa na ukawa unafuata ratiba ya sindano zao kama inavyotakiwa kutwa mara tatu usitegemee Vichaa hao kwamba eti wata appreciate.
 
Utetezi wako kwa Mkurugenzi wa Madini uko dhaifu sana na mbaya zaidi umeshindwa hata ku paraphrase umeleta maneno kama alivyo kutuma, jipange upya,mkurugenzi anaondoka yule
 
Kama

Watu wana hakiya kulipwa, peasa za kulipwa zipo lakini hawalipwi, wameenda kulalamika kwa waziri mwenye dhamana.Kama wengine wanaodai hawalalamiki waziri afanye nini? Si kila anayefanyiwa vibaya kinyume cha maumbile anaenda kushitaki, wengine ndivyo wanavyopenda.
 
Safi sana Kamanda....Nchi Hii CCM wameifanya Shamba La Bibi
 
Kwa muhongo mtapiga sana ramli, naweka mZigo kuwa mbowe na chadema watatumbuliwa kabla ya muhongo.
Ya Makamba yamegonga mwamba mnahamia kwa muhongo.
 
Mnao jisumbua kumkosoa JPM kuwa kakosea kwenye uteuzi wa Baraza lake la Mawaziri, naona mwende kujikalia baa mnywe mchanaa peupeeee. JPM, haongozwi na magazeti.
Hivi, kama angelikuwa anaongozwa na magazeti, Makamba angelikuwa ofisini hadi leo?? Hivi, Simbachawene angelikuwa ofisini hadi leo?? Acheni kupoteza nguvu zenu kumwandikia JPM kumhusu Muongo. Yule, HAGUSIKI kabisaaaa.
Ukiisha kuwa rais, kupitia CCM. Lazima ujifunze kuweka Chama mbele. Chama hakikosei wala hakikosolewi kabisa. Kama rais aliagizwa watu wa kuweka mahali flan, baasi lazima awaweke hapo nao hawatakosea wala kukosolewa na mtu yeyote. Wale mawaziri mizigo mbona wanakula bata mpaka leo.
Msipoteze muda na nguvu zenu bure. Hatoki mtu, awe Muongo au Maropuuuu wala Chawenyewesimba
 
Jipu ambalo nina uhakika nalo ni Muhongo le profeseli ambaye anasemekana ameshindwa kusimamia kikamilifu wizara yake katika maeneo mengi na amekuwa akihusishwa na ugomvi baina yake na wafanyakazi wa wizara na tasisi zilizochini yake.

Muhongo le profeseli ambaye anasemekana (hapa unaonesha huna uhakika na ukiandikacho) ameshindwa kusimamia kikamilifu wizara yake katika maeneo mengi (yataje na jinsi alivyoshindwa) na amekuwa akihusishwa na ugomvi baina yake na wafanyakazi (wataje ili isionekane unatulisha majungu) wa wizara na tasisi zilizochini yake (taja mojamoja na uhusika wake)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…